WAVU KWAENDELEA KUNOGA UMITASHUMTA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Friday, June 13, 2025

WAVU KWAENDELEA KUNOGA UMITASHUMTA



OR-TAMISEMI


Timu ya wasichana kutoka Makao Makuu Dodoma imeonyesha ubabe kwenye mchezo wa wavu kwa kuichapa timu ya wenyeji Iringa kwa seti 3-0.

Dodoma walionyesha kiwango cha juu cha mchezo, wakitawala seti ya kwanza kwa ustadi mkubwa na kuipora Iringa matumaini ya ushindi. Jitihada za Iringa kujibu mashambulizi hazikuzaa matunda baada ya Dodoma kurejea kwa moto zaidi na kushinda seti mbili zilizofuata, na hatimaye kukamilisha ushindi wa seti 3-0.

Katika michezo mingine ya wasichana, Mkoa wa Tabora ulishindwa kuhimili vishindo vya Mtwara na kuambulia kichapo cha seti 0-3, matokeo yaliyoonyesha uimara wa kikosi cha kusini mwa Tanzania.

Kwa upande wa wavulana, mchezo uliovutia kati ya Manyara na Singida uligeuka kivutio baada ya Manyara kuibuka na ushindi mwembamba wa seti 3-2, katika pambano lililoshuhudia ushindani mkali kutoka pande zote mbili.

Katika michezo mingine, Mkoa wa Arusha – wanaoitwa watoto wa kitalii – waliwaliza wachimba madini kutoka Geita kwa kuwachapa kwa seti 3-0, huku Dar es Salaam nao wakijihakikishia pointi tatu muhimu kwa kuifunga Njombe kwa seti 3-0.

Mashindano haya yanaendelea kuvutia hisia kali kutoka kwa wapenzi wa michezo, huku kila timu ikipambana kwa bidii kutafuta nafasi ya kutwaa ubingwa wa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment