WAZIRI WA FEDHA MHE. BALOZI OMAR ATETA NA UONGOZI WA AfDB, - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Friday, April 10, 2026

WAZIRI WA FEDHA MHE. BALOZI OMAR ATETA NA UONGOZI WA AfDB,

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza kikao chake na Ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika, Ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Kanda ya Afrika Bw. Ronald Cafrine, ulipomtembelea katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar Es Salaam.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba (kushoto), akiteta jambo na Meneja wa Benki ya AfDB, Bi. Mary Manneko Monyau, baada ya Kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omari (Mb), na Ujumbe kutoka AfDB, kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar Es Salaam.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiagana na Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, AfDB, Bi. Mary Manneko Monyau, baada ya kikao chake na Ujumbe wa benki hiyo katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar Es Salaam.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (wanne kulia), Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), baada ya kikao chao kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar Es Salaam.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba, akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (hayupo pichani), na Ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Waziri, katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dae Es Salaam.  


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF – Dar Es Salaam)



Na. Asia Singano, WF - Dar Es Salaam


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Afrika, ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Kanda ya Afrika, Bw. Ronald Cafrine, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar Es Salaam.

Katika kikao hicho Mhe. Balozi Mussa Omar pamoja na Ujumbe huo wa Benki ya AfDB, walijadili masuala mbalimbali yanayolenga kuifanya nchi ya Tanzania kufikia malengo yaliyowekwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Akizungumza wakati wa kikao na Ujumbe huo, Mhe. Balozi Omar, aliipongeza benki hiyo kwa hatua mbalimbali za kuzikwamua kiuchumi nchi mbalimbali za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania.

‘’Mkurugennzi ningependa kuchukua fursa hii kuishukuru kwa dhati AfDB kwa ushirikiano na msaada wa masharti nafuu uliyotolewa kwa Tanzania chini ya ADF-16 ambao umekuwa muhimu katika kudumisha kasi katika mipango muhimu ya maendeleo’’ alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kuwa inatambua mchango wa benki hiyo katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ya nishati pamoja na miundombinu mbalimbali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Kanda ya Afrika Bw. Ronald Cafrine, alisema kuwa AfDB inatambua juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kujikwamua kiuchumi hivyo benki hiyo itaendelea kuiunga mkono Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Naye Meneja wa Benki ya AfDB, Bi. Mary Manneko Monyau, alisema amevutiwa na mikakati mbalimbali na mipango ya maendeleo kupitia vipaumbele mbalimbali vilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. inayolenga kuboresha maisha ya wananchi na kukuza uchumi wa Tanzania, hivyo AfDB ipo tayari kuunga mkono juhudi hizo.

Benki ya Maendeleo ya Afrika hivi karibuni imeteua viongozi mbalimbali kwa upande wa Tanzania akiwemo Meneja wa Benki hiyo nchini Tanzania, Bi. Mary Manneko Monyau.

No comments:

Post a Comment