KATIMBA AWAPOKEA WABUNGE WA ZAMBIA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, May 28, 2025

KATIMBA AWAPOKEA WABUNGE WA ZAMBIA


Na OR-TAMISEMI, Dodoma


Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU) Mhe. Zainab Katimba amewapokea wageni kutoka Bunge la Taifa la Zambia ambao wamekuja kutembelea na kujifunza jinsi Mfumo wa Serikali za Mitaa unavyotekelezwa Tanzania Bara.

Akiongea na wageni hao ambao ni Waheshimiwa Wabunge la Taifa la Zambia katika ukumbi wa Sokoine TAMISEMI Jijini Dodoma leo tarehe 28 Mei, 2025 kwa niaba ya Mhe. Mohamed Mchengerwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Katimba alisema Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ndiyo ina mamlaka mapana na muhimu yakiwepo Uratibu na Usimamizi wa shughuli za Serikali ngazi ya Mikoa na Serikali za Mitaa, kujengea uwezo wa Serikali za Mitaa, uendelezaji na utekelezaji wa Sera, upangaji na ufuatilaji wa fedha za Serikali za Mitaa.


Masula mengine ameyataja kuwa ni usimamizi na utoaji wa huduma hasa elimu, afya, na miundombinu, kukuza ugatuaji wa madaraka na utawala bora pamoja na kuwezesha mahusiano baina ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa na utatuzi wa migogoro katika ngazi ya Halmashauri na ngazi ya msingi pamoja na utoaji wa huduma kwa wananchi.

“majukumu haya ni muhimu katika kuhakikisha maendeleo jumuishi, uboreshaji wa utoaji wa huduma kwa wananchi, na utawala shirikishi – maadili tunayoamini yanashirikishwa katika nchi zetu zote mbili” alisisitiza Mheshimiwa Katimba.

Akiongea kwa niaba ya Waheshimiwa Wabunge wenzake, Mheshimiwa Twaambo Mutinta (Mb), Mkuu wa Msafara na Mwenyekiti wa Kamati ya Serikali za Mitaa, Makazi na Masuala ya Machifu (Chiefs’ Affairs) alishukuru kwa mapokezi mazuri yaliyofanywa na ofisi ya Rais - TAMISEMI na kusema nchini Zambia Mfumo wa Ugatuaji wa Madaraka ulianza mwaka 2016 na hivyo watakuwa na wakati mzuri wa kujifunza hapa Tanzania na kubadilishana ujuzi kwani umuhimu mkubwa unaonekana katika kupeleka rasilimali na maamuzi karibu na wananchi haya yote ni moja ya vitu ambavyo tunatarajia tutashirikishwa katika ziara hii.

Naye Angelista Kihaga Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa Ofisi ya Rais TAMISEMI akiwasilisha mada kwa ugeni huo, amesema Idara ya Serikali za Mitaa ni moja ya idara za Ofisi ya Rais -TAMISEMI ambayo inalo jukumu kubwa la kuratibu na kusimamia kazi za Mamlaka za Serikali za MitaaTanzania Bara. Idara hiyo ina sehemu tatu ambazo ni sehemu ya Usimamizi wa Rasilimali Fedha katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sehemu ya Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa na Sehemu ya Usimamizi wa Utoaji Huduma na Utawala Bora katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Kihaga aliongeza kuwa Halmashauri zinafanya kazi chini ya Mfumo wa Ugatuzi wa Madaraka (Decentralization by Devolution) lakini zinakuwa na uhusiano wa karibu na Serikali Kuu kupitia mwelekeo wa kisera, usaidizi wa kifedha na uangalizi wa kiutawala unaotolewa na Ofisi ya Rais TAMISEMI lakini pia Sekta na wizara nyingine. Serikali kuu inaziongoza Halmashauri katika kupanga mipango na bajeti, utoaji wa huduma na ufuatiliaji wa utendaji wao kupitia Sekretarieti za Mikoa

Halmashauri zinajumuisha timu za Usimamizi wa Halmashauri (CMTs) zikiongozwa na mkurugenzi anayeunda sehemu ya Wataalaam na sehemu nyingine inayoundwa na Waheshimiwa Madiwani ambapo kwa pamoja huunda Baraza. Aidha, kuna Madiwani wa kuchaguliwa kutoka kwenye Kata na kutoka Viti Maalum na Halmashauri kamili ndiyo wanaotoa maamuzi ya mwisho katika baraza hilo.

No comments:

Post a Comment