
Timu ya Mpira wa Mikono (Handball) Wasichana kutoka Mkoa wa Mara, imeshinda mchezo wa nne mfululizo katika mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa Shule za Msingi yanayoendelea mkoani Iringa.
Katika mchezo uliochezwa leo tarehe 13 Juni 2025 kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Iringa Wasichana, Mkoa wa mara uliibuka na ushindi mnono baada ya kuifunga Pwani magoli 26-12.
Kwa matokoe hayo sasa timu ya mkoa wa Mara inaongoza kundi C, ikiwa imebakiwa mchezo mmoja dhidi ya Shinya, huku timu zingine katika kundi hilo zikiwa ni Morogoro Iringa na Dodoma.
Katika michezo mingine ya Volleyball Wasichana iliyochezwa asubuji ya leo, Tanga iliifunga Ruvuma magoli 10-0, na Mbeya ikatoshana nguvu ya magoli 10-10 dhidi ya Katavi.
Upande wa Wavulana, timu ya Mkoa wa Arusha ilikubali kipigo cha magoli 15-6 kutoka kwa Njombe kwenye mchezo wa awali uliochezwa kwenye uwanja huohuo wa Shule ya Sekondari Wasichana Iringa.
Mashindano ya UMITASHUMTA yaliyofunguliwa rasmi tarehe 9 Juni 2025 na WaziriMkuuMh.Kassim Majaliwa, yanaendelea kushika kasi katika viwanja vya Kichangani, Shule ya Sekondari Lugalo,Shule ya Sekondari Wasichana Iringa na Chuo cha ualimu Kleruu.

No comments:
Post a Comment