
Michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam yaani Azam Sports Federation Cup (ASFC), inaendelea kesho Alhamisi Novemba 9, 2017 kwa michezo saba ambako Dar City itacheza na Majimaji Rangers ya Lindi.
Mashujaa ilikwisha kupata mpinzani ambaye ni Buseresere ambaye kabla aliifunga Isoko katika hatua ya awali. Mchezo huo utafanyika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.
The Mighty Elephant itacheza na Makanyagio kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea. Namungo na Villa Squad nazo zinacheza kesho kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara .
No comments:
Post a Comment