![]() |
Waendesha pikipiki maarufa kama Bodaboda Mkoani Dodoma
wametakiwa kuyatendea kazi mafunzo wanayoyapata juu ya usalama barabarani ili
kuunga mkono serikali katika kupunguza ajali za barabarani.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa chuo cha WIDE INSTITUTE OF DRIVING chenye
makao yake makuu mkoani Kilimanjaro ambayr ndiye Mkufunzi mkuu wa mafunzo hayo
Ndugu FAUSTIN
MATINA wakati akifunga
mafunzo hayo yaliyodumu takaribani wiki mbili katika kata ya SONGOLO wilayani
CHEMBA yenye lengo la kuwafanya madereva pikipiki kujua haki zao na kuepuka
uvunjifu wa Sheria za barabarani bila kujua.
Pia ameelezea masikitiko yake kwa baadhi ya wahitimu wa
mafunzo hayo kuendelea kutenda makosa barabarani hata baada ya kupata elimu
pamoja na leseni ambazo hutolewa kwa ushirikiano mkubwa ulipo kati yao na
TRA pamoja na Jeshi la polisi kupitia
kitengo cha usalama barabarani kudai kuwa hayo ni makusudi.
“Inasikitisha sana kuona madereva waliohitimu mafunzo
wanaendelea kufanya makosa barabarani
hivyo kwa nyie mnaohitimu leo nawaomba mkayazingatie haya ili kuepukana
na ajali zinazozuilika” alisema Faistin Matina
Kwa upande wake Afisa huduma na elimu kwa mlipa kodi mkoa wa
Dodoma Barnabas
John Masika amewapongeza waliohitimu mafunzo hayo kwa muitikio wao
katika kupata elimu hiyo ya usalama Barabarani na kusema mbali na kupata elimu
hiyo watakuwa walipa kodi na kuliongezea mapato taifa.
Pamoja na hayo wahitimu hao wametakiwa kuweka akiba ili
kuweza kuondokana na umasikini pamoja na kujiingiza katika fursa nyingine ili
kuweza kujipatia pesa zaidi kwa sababu hshima ya kwanza duniani ni pesa.
"Kama huna pesa ndugu yangu hakuna lolote heshima hakuna kwa hivyo jaribu kuhakikisha unaweka akiba na mjitahidi kujiingiza kwenye biashara pia ili muweze kuongeza kipato chenu"Aliongeza Faustin Matina
Wakizungumza kwa
niaba ya wahitimu wote ALLY RASHID MWAHU kutoka kituo cha Kondoa Mjini amesema
mafunzo haya lazima yazingatiwe wakati AMMY ADULLAH ISUMBULA kutoka kituo cha
Chemba yeye kwa upande wake amesema kuwa atawahamasisha wale ambao hawajitokeza
katika kupata mafunzo hayo ili nao wajitokeze katika kipindi kingine.
Pamoja na hayo wametoa ushauri kwa Mkuu wa chuo cha WID INSTITUTE OF DRIVING kuwa wajitahidi kuja katika kipindi ambacho wakulima wamkwishavuna mazao ya ili kutoa fursa kwa watu wngi kushiriki katika mafunzo hayo.
Mafunzo hayo
yanaendelea katika wilaya ya CHEMBA pamoja na KONDOA katika kata mbalimbali na
lengo kubwa ni kuiunga mkono serikali ya awamu ya tano katika kampeni ya
kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua ama kumalizika kabisa.
HABARI PICHA;
HABARI PICHA;
![]() |
Maandamano ya waendesha pikipiki kutoka Goima hadi SONGOLO Wilayani CHEMBA (Picha na Okuly Julius) |
![]() |
Wahitimu katika kituo cha KONDOA MJINI Wakiwa na wakufunzi wao katika picha pamoja baada ya kufungwa kwa mafunzo.(Picha na Okuly Julius} |
![]() |
Wahitimu wakiwakatika picha ya pamoja na wakufunzi wao baada yakufungwa kwa mafunzo katika kituo cha KONDOA MJINI .(Picha na Okuly Julius) |
![]() |
Dereva Bodaboda kutovaa kofia ngumu (HELEMENT) ni makusudi tuu. |
![]() |
wanafunzi katika kitua cha SONGOLO wilayani Chemba(Picha na Okuly Julius) |
No comments:
Post a Comment