Na Okuly Julius Dodoma
Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa CCM mkoa wa Dodoma Billy Chidabwa amewashauri vijana kujikita katika kilimo kwa sababu kilimo ndiyo uchumi wa mwanadamu.Akizungumza mara baada ya kutembelea kiwanda cha mbolea intrakom kilichopo kata ya zuzu mkoani Dodoma, chidabwa amesema kuwa kiwanda hicho ni fursa tosha kwa vijana hivyo wanapaswa kujikita kwenye kilimo ili waendane na uwekezaji huo kiwanda kwa maslahi ya Taifa na watu wake.
Aidha,Mwenyekiti huyo ametoa Rai kwa serikali kuhakikisha wanapeleka miundombinu rafiki katika kiwanda hicho Hususani umeme na maji ili viendane na ukubwa wa kiwanda hicho.


No comments:
Post a Comment