![]() |
| Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa Dkt. Edimund Mndolwa,akizungumza wakati wa kikao cha tathmini na Wakuu wa Shule za Jumuiya ya Wazazi kilichofanyika leo Julai 15, 2022 jijini Dodoma. |
![]() |
| Katibu Mkuu wa Jumuiya Ya Wazazi Bw.Gilbert Kalima ,akizungumza wakati wa kikao cha tathmini na Wakuu wa Shule za Jumuiya ya Wazazi kilichofanyika leo Julai 15, 2022 jijini Dodoma. |
Na Okuly Julius-Dodoma
Chongolo amebainisha hayo leo Juni 15,2022 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa semina ya watumishi wa taasisi za elimu zinazomilikiwa na jumuiya ya wazazi ya chama hicho.
Chongolo amesema lengo la chama kuanzisha shule ni kuwezesha vijana wote kupata elimu iliyobora ambapo katika matokeo ya mtihani mwaka huu karibu asilimia 80 hadi 90 ya wanafunzi wanaosoma katika shule zinazomilikiwa na chama wamepata ufaulu wa daraja la kwanza na la pili huku mwanafunzi mmoja tu akipata ufaulu wa daraja la nne.
Aidha,ametoa wito kwa jumuiya kuendelea kuwajengea uwezo viongozi wa shule ili heshima ya wakuu wa shule iendane na muda aliokaa katika shule.
Hata hivyo,amesisitiza kwa wakuu wa shule kuendelea kujenga nidhamu katika shule wanazoziongoza katika kuendelea kujenga heshima ya chama.
Katika hatua nyingine amebainisha kuwa heshima ya mwalimu ni matokeo bora hivyo amesisitiza kuwa awamu ijayo watatoa zawadi kulingana na kiwango cha ufaulu katika shule husika na kuwataka walimu kukaza buti katika ufundishaji.
Mwenyekiti jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi [CCM] Dkt.Edmundi Mndolwa amewataka watumishi katika taasisi za elimu zinazomilikiwa na chama kuacha kujihusisha na masuala ya siasa bali kujikita zaidi katika ufanikishaji wa utoaji wa elimu Bora.
Aidha,amesema kiwango cha ufaulu katika shule zinazomilikiwa na Chama zimeendelea kuimarika siku hadi siku kwani hakuna shule yoyote iliyopata daraja sifuri.







No comments:
Post a Comment