Kagera Sugar ilianza kupata bao kupitia kwa nyota wao Deus Bukenya dakika ya 15 kabla ya Henock Inonga ajasawazisha dakika ya 38 yaa mchezo na kuwapeleka mapumziko ubao ukisoma 1-1.
Kwa matokeo hayo Simba Sc wamendelea kubaki nafasi ya pili wakiwa na Pointi 38 wakizidiwa pointi 6 na Vinara Yanga wenye Pointi 44.
Michezo mingine iliyochezwa leo Tanzania Prisons wameutumia vyema uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kwa kuichapa Dodoma jiji mabao 2-0.
Timu ya Geita Gold imeshindwa kutamba katika uwanja wao wa Nyankumbu Girls kwa kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na Azam FC huku Azam wakibaki nafasi ya tatu akiwa na pointi 37.
No comments:
Post a Comment