Tanzania mikononi mwa Mama, Kauli hii inamaanisha kama taifa tunaendelea kujivunia mengi na makubwa yaliyotekelezwa na yale yanayoendelea kutekelezwa Chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Ni mikaa miwili tu, Rais Samia amekamilisha ujenzi wa Zahanati 1,066, ujenzi wa Hospitali za wilaya 135, Hakuacha majengo tu akapeleka na Vifaa tiba vya kutosha.
Hatusemi ilimradi tumesema, Mama amejenga vituo vya afya 234 kupitia Tozo tu, huku vituo vya Afya 74 vimejengwa kupitia fedha za Ruzuku, na kama haitoshi kupitia mapato ya ndani vituo vya Afya 90 vimejengwa, akapeleka na vifaa tiba kwaajili ya Vyumba vya Upasuaji, Mionzi, Maabara.
Kama hiyo haitoshi Dkt. Samia ameboresha huduma za ‘AfyaMsingi’ na kuwezesha ujenzi wa majengo 80 ya dharula yaani ”EMD’’ Majengo ya kuhudumia wagonjwa mahututi yaani ICU 28, Ujenzi wa nyumba za watumishi 450
Aidha alitoa fedha za kusimika mitambo 21 ya Kuzalishia hewa safi kwa binadamu yani Oxygen, na kuajiri watumishi wa Afya zaidi ya 10,324 hii inamaanisha kwenye eneo la Afya imetumika Zaidi ya Bilioni 600 za kitanzania kwaajili ya maboresho yote.



No comments:
Post a Comment