Ofisi ya vyombo vya habari vya serikali ya Gaza inayoongozwa na Hamas imesema Wapalestina 18 wameuawa walipokuwa wakijaribu kukusanya misaada inayohitajika sana ambayo ilirushwa kaskazini mwa Gaza.
Watu kumi na wawili walikufa maji walipoingia baharini kuchukua vifurushi vya chakula, wengine sita walikanyagwa hadi kufa katika "mikanyagano" wakati vifurushi vingine vya misaada vilitua chini, taarifa ilisema.
Inataka "kukomeshwamara moja" kwahatua ya kutupwa kwa vyakula kupitia angani, na kuiita "ya kukera, mbaya,isiyofaa".
Video, iliyopatikana na Reuters, imeibuka ya Wapalestina waliokuwa wakikimbilia pwani baada ya misaada kuangushwa kwenye ufuo karibu na mji wa kaskazini wa Beit Lahia siku ya Jumatatu.
Inaonyesha watu wakikimbia huku dazeni za vifurushi vya misaada vilivyowekwa kwenye miamvuli vikielea chini karibu na pwani.
Israel - ambayo iko chini ya shinikizo kuruhusu misaada zaidi kuingia Gaza kupitia ardhi - inasema iliwezeshavifurushi vyatani 159 za misaada kaskazini mwa Gaza siku ya Jumatatu.
Marekani inasema ndege mbili aina ya C-17 zilidondosha "miloiliyotayari kuliwa" 46,000 (MREs) kaskazini siku ya Jumatatu, huku Uingereza ikisema moja ya ndege zake aina ya A400M ilidondosha tani 10 za maji, mchele, mafuta ya kupikia, unga,vinywaji vya Watoto.
Mashirika ya kibinadamu yameonya kuwamisaada inayorushwa kwa njia hiyo haiwezikukidhi hitaji kubwa la chakula na mkakati huo umezua mjadala mkubwa.
No comments:
Post a Comment