MWENENDO WA UREJESHAJI MIKOPO KWENYE HALMASHAURI UNARIDHISHA - DKT. DUGANGE - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Thursday, May 8, 2025

MWENENDO WA UREJESHAJI MIKOPO KWENYE HALMASHAURI UNARIDHISHA - DKT. DUGANGE



OR - TAMISEMI


Serikali kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI imesema mwenendo wa urejeshaji wa mikopo yote iliyotolewa kwa vikundi vya wanawake, wajasiliamali, watu wenye ulemavu na vijana kabla ya Aprili 2023 ni wenye kuridhisha na Serikali imeendelea kusimamia ili kuhakikisha pesa yote iliyokopeshwa inarejeshwa.

Hayo yamesemwa leo Mei 08, 2025 bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati akijibu swali la msingi la Mheshimiwa Mwantumu Haji Mbunge wa Viti Maalum aliyetaka kujua ni lini Serikali itaanza kuwapatia Mikopo Wajasiriamali Wadogo Wanawake na Vijana.

Katika majibu yake Naibu Waziri Dkt. Dugange amesema, Serikali ilifanya tathimini juu ya utaratibu wa mwanzo uliokuwa ukitumika kutoa na kurejesha mikopo na ilibaini uwepo wa mianya ya kufanya vikundi kutorejesha mikopo kwa ufanisi na kwa wakati unaotakiwa ndiyo maana serikali ilisitisha mikopo hiyo na kuandaa kamati mpya, utaratibu na kanuni kwa ajili ya kusimamia mikopo hiyo katika maeneo yote ya halamashauri.

“Mheshimiwa Spika, Serikali ilisitisha kwa muda utoaji wa mikopo ya asilimia 10 katika mamlaka za serikali za mitaa Aprili 2023 kwa lengo la kufanya maboresho. Aidha, mikopo hii ilianza kutolewa tena tarehe 01 Julai, 2024 kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa na Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu za mwaka 2024” alisema Naibu Waziri Dkt. Dugange.


Aidha aliongeza kuwa “Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2024/25, Serikali kupitia halmashauri ilitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 82.84 kwa vikundi 8,275 vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 40.71 zilitolewa kwa vikundi vya wanawake, shilingi bilioni 36.64 kwa vikundi vya vijana, na shilingi bilioni 5.48 kwa vikundi vya watu wenye ulemavu”.Amefafanua Mhe. Dugange

No comments:

Post a Comment