Angela Msimbira MANYARA
Serikali kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na shirika la Imagine imezindua rasmi mradi wa MsingiTek utakaotekelezwa katika mikoa 5 na halmashauri 10, ukihusisha shule 500 za Tanzania Bara.
Akiongea kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu Atupele Mwambwene, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Elimu Bi.Suzan Nussu amesema lengo la mradi ni kuboresha stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) kwa madarasa ya awali (darasa la I–III), kwa kutumia vishikwambi vyenye programu maalum zinazomsaidia mwanafunzi kujifunza kwa njia shirikishi na ya kuvutia.
Ameendelea kufafanua kuwa mradi wa msingTek utarahisisha kazi ya ualimu, kupunguza utoro, na kuongeza motisha kwa wanafunzi.
Pia amewaelekeza viongozi wa sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kushirikiana kwa karibu na walimu kuhakikisha mradi huo unafanikiwa na kuweza kupanuliwa zaidi.
No comments:
Post a Comment