
Meneja wa Tottenham Thomas Frank anataka kuungana tena na mshambuliaji wa Al-Ahli na England Ivan Toney mwenye umri wa miaka 29 - ambaye alicheza chini yake katika klabu ya Brentford. (Sportsport)
Mshambuliaji wa Real Madrid wa Brazil Rodrygo, 24, pia yuko kwenye orodha ya washambuliaji wanaolengwa na Tottenham. (Teamtalk)
Arsenal imeweka thamani ya euro 150m (£132m) kwa kiungo wa kati wa Uingereza Declan Rice, 26, ambaye anashangiliwa na Real Madrid. (Fichajes - kwa Kihispania)
Chelsea imeulizia mchezaji wa Como Nico Paz, 21, lakini inakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Real Madrid, ambao wanaweza kutaka kumsajili tena kiungo huyo wa Argentina. (TBR Football)
Newcastle "haijatoa" tamko lolote baada ya kauli ya Sandro Tonali kuhusu mustakabali wake, na hhaitaanza mazungumzo rasmi kuhusu mkataba mpya wa kiungo huyo kimataifa wa Italia mwenye umri wa miaka 25 hadi baadaye msimu huu. (Mail Plus - usajili unahitajika)
Napoli huenda ikafufua nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United na Uingereza Kobbie Mainoo, 20, mwezi Januari. (Calciomercato - kwa Kiitaliano)

No comments:
Post a Comment