SERIKALI YASISITIZA USALAMA NA MAPATO MPAKANI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, December 23, 2025

SERIKALI YASISITIZA USALAMA NA MAPATO MPAKANI


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amehimiza ushirikiano kati ya watumishi wa serikali waliopo katika Kituo cha Forodha cha Pamoja cha Mutukula kilichopo wilayani Misenyi mkoani Kagera ambapo ni mpaka kati ya nchi ya Tanzania na Uganda huku akiwaasa kutilia mkazo masuala ya usalama na ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo ya nchi ambapo uhitaji wa usalama na mapato ni muhimu ili nchi iweze kukua kiuchumi.

Ametoa rai hiyo wakati wa ziara ya ukaguzi wa shughuli mbalimbali za kiforodha katika kituo hicho akiambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Kagera ambapo awali alipowasili mkoani humo alipata ripoti ya hali ya ulinzi na usalama kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera,Hajjat Fatma Mwassa,ripoti iliyoonyesha kuwepo kwa sintofahamu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo ikiwemo wingi wa vipenyo vinavyotumiwa na wahamiaji haramu na watu wanaoweza kuingia nchini kwa nia ovu ya kuvuruga amani iliyopo.

‘Kwanza ni usalama wa nchi yetu, kwahiyo kila mmoja aliyepo huku jambo namba moja ni usalama wa nchi yetu, lakini la pili ni ukusanyaji wa mapato,ili nchi iweze kuendelea inahitaji fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo imeahidiwa kwa wananchi na hiyo fedha ya kuendeleza miradi hiyo inapatikana kwenye maeneo ya ukusanyaji, moja kati ya maeneo muhimu ni mipakani, mpaka huu wa mutukula kati ya Tanzania na Uganda ni sehemu ambayo tunaamini makusanyo yakifanyika vizuri yatasaidia kutunisha mfuko wa serikali ili kuweza kufanikisha miradi inayohudumia wananchi zikiwemo huduma za afya,miundombinu kama Barabara,shule na kilimo.’ Alisema Simbachawene

No comments:

Post a Comment