Bado headlines za usajili wa dirisha 
dogo bado zinachukua nafasi kwa wachezaji kadhaa kuhusishwa kujiunga na 
vilabu fulani na wengine kutemwa na vilabu vyao kutokana na 
kutoridhishwa na viwango vya wachezaji hao. November 18 klabu ya Simba 
imetangaza kuwatema wachezaji wawili wa kimataifa.
Simba ambayo ilikuwa inatajwa kwa karibu
 kumtema Pape N’daw aliyetokea Senegal na mchezaji mmoja mwingine wa 
kigeni, imethibitisha leo November 18 kuwatema wachezaji wawili Simon 
Sserunkuma kutoka Uganda na Pape N’daw kutokea Senegal aliyeitumikia 
klabu hiyo kwa nusu msimu na kocha wa Simba Dylan Kerr kupendekezwa 
aachwe kutokana na kutoridhishwa na uwezo wake.
Kupitia kwa Afisa Habari wake Haji 
Manara wametangaza kuwatema wachezaji hao na kumrejesha Paul Kiongera 
aliyekuwa anaichezea KCB ya Kenya kwa mkopo. Hata hivyo mmoja kati ya 
wanachama wa Simba amemleta mchezaji kutoka Cameroon Doumbie 
Ernest usiku wa November 17 kwa ajili ya majaribio Simba.
“Simba
 imeachana na Pape N’dawa na Simon Sserunkuma kutokana na mapendekezo ya
 benchi la ufundi hususani mwalimu Kerr ila katika kuacha huko Simba 
inamrejesha mchezaji wake Paul Kiongera aliyekuwa kwa mkopo KCB ya Kenya
 na inaweza kusajili mchezaji mwingine 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment