Washambuliaji wawili wa TP Mazembe,
Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanatarajia kutua jijini Dar es Salaam, leo.
Samatta
 na Ulimwengu wataungana na Stars leo jioni kwa kuwa kikosi hicho 
kinatarajia kutua jijini Dar es Salaam leo saa 12 jioni kikitokea Afrika
 Kusini kilipoweka kambi ya zaidi ya wiki moja.
Samatta
 na Ulimwengu walikuwa DR Congo ambako waliiongoza TP Mazembe kubeba 
ubingwa wa Afrika na kuwa Watanzania wa kwanza kuvaa medali ya Ligi ya 
Mabingwa Afrika.
Stars
 utawasili hiyo jioni kwa ndege ya Fast Jet na moja kwa moja itakwenda 
kambini kufanya maandalizi ya mwisho kwa ajili ya mechi dhidi ya Algeria
 itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumamosi.

No comments:
Post a Comment