Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Kaunti ya Kiambu, Mohamed Badel amesema watuhumiwa hao, hufurika katika mitaa ya Mji wa Kiambu kuanzia majira ya saa kumi alfajiri hadi saa kumi na moja, muda ambao watu wengi hutoka majumbani mwao kuelekea makazini.
Badel amesema waliamua kuendesha oparesheni maalum baada ya kusikia malalamiko ya mara kwa mara ya wakazi wa mji huo ambapo kwa kushirikiana na wasamaria wema, walifanikiwa kuwanasa wahalifu hao.
Ameongeza kuwa watuhumiwa wote wapo rumande na wanatarajiwa kufikishwa katika Mahakama ya Kiambu kusomewa mashtaka yanayowakabili na kuwataka madereva wa bodaboda wanaozingatia sheria, kujiandikisha na kupewa namba maalum zitakazowatofautisha na wahalifu.
Pia amewataka watu walioibiwa simu zao, kufika katika Kituo cha Polisi cha Kiambu ili kuzitambua simu zao.
No comments:
Post a Comment