TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA[TAEC] WAKAA KIKAO CHA PAMOJA NA WADAU KUPITIA MAPENDEKEZO YA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA TOZO - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Monday, February 14, 2022

TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA[TAEC] WAKAA KIKAO CHA PAMOJA NA WADAU KUPITIA MAPENDEKEZO YA MAREKEBISHO YA KANUNI ZA TOZO





Na ,Okuly Julius, Dodoma

Tume ya nguvu za atomiki Tanzania [TAEC]kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara wamekaa kikao cha Pamoja  cha kupitia mapendekezo ya marekebisho  na maboresho  ya Kanuni za  tozo .

Akizungumza  katika ufunguzi wa kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi idara ya Sayansi,Teknolojia na Ubunifu  kutoka Wizara ya Elimu ,Sayansi  na Teknolojia  Dkt.Alexander Mtawa amesema kikao hicho kitasaidia kuleta maboresho ya kanuni za nguvu za atomiki nchini.

Kwa upande wake mkurugenzi Mtendaji Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania[TAEC]Prof.Lazaro Busagala amebainisha malengo ya kikao hicho ni pamoja  kujadili namna ya  kuwalinda wananchi wasidhurike na madhara yatokanayo na mionzi.

Pamoja na hayo Prof.Lazaro Busagala ameongeza kuwa wafanyabiashara wadogo hawatokuwa wanalipa tozo na badala yake watakuwa wanapata huduma kwa ubora uleule.

Hata hivyo amewataka wafanyabiashara kujisajili katika Tume ya nguvu za atomiki Tanzania (TAEC) ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo yao ikiwa ni ndani na nje ya nchi.

Akiwahakikishia Watanzania  kuwa mpaka sasa hakuna tukio lililoripotiwa la madhara yatokanayo na mionzi kwa sababu Tume hiyo ipo makini katika kuhakikisha usalama wa Watanzani katika nyanja hiyo ya mionzi.

Mmoja wa wadau hao,Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya usafirishaji wa bidhaa Tanzania Exporters Association [TANEXA ]Peter Lanya amezungumzia manufaa watakayopata kutokana na maboresho ya kanunihizo,ikiwemo urahisishwaji katika usafirishaji wa mizigo kwa upande wao kama wafanyabiashara itawasaidia sana.

Ikumbukwe kuwa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania[TAEC]ilianzishwa kwa sharia ya Bunge  Na.7 ya mwaka 2003 na hapo awali ilikuwa ikijulikana kama Tume ya Taifa ya Mionzi  iliyoanzishwa kwa sharia ya Bunge Na.5 ya mwaka 1983  na miongoni mwa majukumu yake ni kudhibiti matumizi salama ya mionzi nchini,kuhamasisha na kuendeleza matumizi salama ya Teknolojia ya Nyuklia na kufanya utafiti  na kutoa ushauri na taarifa mbalimbali juu ya Sayansi na Teknolojia ya Nyuklia.










No comments:

Post a Comment