Wananchi Wapewa Kilomita za Mraba 2,500 Pori la Loliondo - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Sunday, June 12, 2022

Wananchi Wapewa Kilomita za Mraba 2,500 Pori la Loliondo




Serikali inayoongozwa na Rais

Samia Suluhu Hassan imetenga

eneo lenye ukubwa wa kilomita za

mraba 2,500 lililopo kwenye Pori

Tengefu la Loliondo kwa ajili ya

makazi ya wananchi.


Hayo yameelezwa huko

Loliondo mkoani Arusha na Mkuu

wa Mkoa huo, Mhe. John Mongella alipotembelea eneo hilo.


“Uongozi wa mkoa, uongozi wa

wilaya na vyombo vyetu vya ulinzi

na usalama tupo Loliondo, hali ni

shwari na kama mnavyojua

tunaendelea na zoezi la kuweka

mipaka kwenye eneo la pori

tengefu la Loliondo ambalo lina

kilomita za mraba 1,500.


“Na kama mtakumbuka kuwa kwa

mujibu wa sheria eneo ambalo ni

pori tengefu ni kilomita za mraba

4,000 lakini Serikali kwa makusudi

kabisa kwa kujali shughuli za

wananchi sasa imetenga kilomita

za mraba 2,500 kwa ajili ya wananchi kuendelea na shughuli zao.


“Na kilomita 1,500 za mraba kwa

ajili ya uhifadhi wa eneo nyeti la

mazalia ya wanayama, njia zao na

vyanzo vya maji, eneo hilo ndio

chanzo kikuu cha maji kwenye

Hifadhi ya Serengeti, Ngorongoro

na Hifadhi ya Masai Mara iliyopo

Kenya,” ameeleza Mkuu wa Mkoa.
    
 CHANZO NI MAELEZO 

No comments:

Post a Comment