NACTVET INAKUKARIBISHA KATIKA DAWATI LAO LILILOPO KWENYE BANDA LA JAKAYA KIKWETE KUPATA HUDUDUMA MABALMBALI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, July 6, 2022

NACTVET INAKUKARIBISHA KATIKA DAWATI LAO LILILOPO KWENYE BANDA LA JAKAYA KIKWETE KUPATA HUDUDUMA MABALMBALI


Na mwandishi wetu Dar-es-salaam

Wageni wanaotembelea Maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama DITF yanayofanyika Viwanja vya Saba Saba, barabara ya Kilwa, wanaendelea kupatiwa huduma mbali mbali kwenye dawati la NACTVET lililomo ndani ya Banda la Jakaya Kikwete.

Mratibu Mwandamizi kutoka NACTVET, bi.Levina Lunyungu (pichani) anaendelea kutoa huduma kwa wageni wanaohitaji namba ya uthibitisho wa tuzo (AVN) ikiwa ni moja kati ya huduma nyingi zinazotolewa katika Banda hilo

Wakati huohuo Wanafunzi wengi waliomaliza masomo ya stashahada wanaotaka kuendelea na masomo ya shahada nao wanatembelea Banda la NACTVET kupata huduma hiyo.

Aidha, wananchi wengi wanaotembelea Maonesho hayo yaliyoanza tarehe 28 Juni 2022 wanapata maelezo mbalimbali kuhusu majukumu ya Baraza na huduma zingine ikiwemo namna ya kuanzisha chuo cha ufundi cha kati na vile vile wanapatiwa mwongozo kuhusu hatua za kuanzisha Chuo cha ufundi stadi (VTC).

No comments:

Post a Comment