NACTVET YATIA KAMBI MAONESHO YA 17 YA ELIMU YA JUU,SAYANSI NA TEKNOLOJIA KARIBU UPATE HUDUMA. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, July 19, 2022

NACTVET YATIA KAMBI MAONESHO YA 17 YA ELIMU YA JUU,SAYANSI NA TEKNOLOJIA KARIBU UPATE HUDUMA.


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) linashiriki kikamilifu Maonesho ya 17 ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, yaliyoanza tarehe18/7/2022 kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja – Dar es Salaam.

Idadi ya wageni 42 wametembelea Banda la NACTVET siku ya kwanza ya maonesho hayo ili kujielimisha juu ya udahili, na kupata huduma ya Namba ya uthibitisho wa tuzo (AVN) na wengine kujua namna ya kuanzisha vyuo vya kutoa ujuzi kwa muda mfupi kwa mfumo wa vituo vya mafunzo ya ufundi stadi.

Maonesho hayo ambayo Kauli mbiu yake ni: Elimu ya Juu Inayokidhi Mahitaji ya Soko la Ajira kwa Maendeleo ya Kijamii na Kiuchumi yamefunguliwa rasmi leo tarehe 19/7/2022 na waziri mkuu Kassim Majaliwa.

                     NACTVET inakukaribisha kupata huduma !

No comments:

Post a Comment