WIZARA YA ELIMU YATOA TUZO KWA WAANDISHI WA HABARI MAHIRI WA SEKTA YA ELIMU. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, December 20, 2022

WIZARA YA ELIMU YATOA TUZO KWA WAANDISHI WA HABARI MAHIRI WA SEKTA YA ELIMU.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe.Nape Nnauye akimkabidhi tuzo Okuly Julius kutoka OKULY BLOG iliyotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia baada ya kutambua mchango wake katika kuripotihabarizaSektayaElimu, SayansinaTeknolojiakwamwaka 2022 .Tuzo hiyo imetolewa katika Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari mwaka 2022 lililofanyika Disemba 17,2022 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, Jijini Dar-es-salaam.
Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi Mkuu wa idara ya Habari Maelezo Gerson Msigwa (kushoto) na Mkurugenzi msaidizi Idara ya Habari MAELEZO Zamaradi Kawawa (kulia) katikati pucha ya pqmoja na Mshindi wa Tuzo iliyotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Okuly Julius  (katikati) baada ya kutambua mchango wake katika kuripoti habari za Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka 2022.Tuzo hiyo imetolewa katika Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari mwaka 2022 lililofanyika Disemba 17,2022 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, Jijini Dar-es-salaam.
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknojia Sylvia Lupembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa tuzo zilizotolewa na wizara hiyo waandishi wa habari waliofanya vizuri katika kuripoti habari za Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka 2022 na Tuzo hizo zimetolewa katika Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari mwaka 2022 lililofanyika Disemba 17,2022 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, Jijini Dar-es-salaam


Na Okuly Julius-Dodoma

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetumia vyema Kongamano la Kwanza la Maendeleo ya Sekta ya Habari mwaka 2022 ,kwa kutoa tuzo za kutambua mchango kwa waandishi wa habari katika kuripoti habari za Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka 2022.

Kongamano hilo lililobebwa na kauli mbiu isemayo "Habari kwa Maendeleo Endelevu " liliwakutanisha zaidi ya Wadau 1000 kutoka Sekta ya habari Disemba 17,2022 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, Jijini Dar-es-salaam na kufunguliwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe.Nape Nnauye.

Ambapo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetoa tuzo kwa waandishi waandishi watano(5) kutambua mchago wao katika kuandika na kuziripoti habari mbalimbali za Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa Mwaka 2022.

Waandishi hao watano waliopata tuzo ni pamoja na Kuringe Mongi - Channel Ten,Jacob Mosenda- Citizen,Okully Julius- Okully Blog, Safina Yasir -TBC One na Mwamini Andrew -TBC Taifa Radio.

Akizungumza mara baada ya utoaji wa tuzo hizo Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknojia Sylvia Lupembe amesema kuwa tuzo hizi zitasaidia kuamsha hamasa kwa waandishi kuandika habari nyingi za sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

"napenda kusema tunatambua na kushukuru waandishi wote ambao hakika wana saidia utoaji habari za Sekta, katika tukio hili la kwanza tumetambua wachache lakini wote kwetu wanastahili ." amesema Sylvia

Pia Sylvia ameongeza kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatambua vyema mchango wa waandishi na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini hivyo wataendelea kuto ushirikiano mkubwa ili kuendelea kuijuza hadhira ya watanzania mambo mazuri yanayoendelea katika Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

"tutaendelea kushirikiana nanyi milango yetu iko wazi na tutaimarisha zaidi utoaji taarifa si tu za matukio lakini hata majibu na maelezo pale waandishi watakapohitaji. "amesema Sylvia

Akizungumza kwa niaba ya washindi hao Okuly Julius kutoka Okuly Blog ameishukuru Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia kwa kumpatia tuzo hiyo huku akitafsiri kuwa ni heshima kubwa kwake na kuahidi kuendelea kuongeza kasi katika kuripoti na kutoa habari za Sekta ya Elimu ,Sayansi na Teknolojia.

"Tuzo hii ni kama imeniamsha upya kwa sababu kila mwandishi angetamani kuipata ila Wizara hii kupitia Kitengo cha Mawasiliano Serikalini imeona ni vyema kuniamini na kunipatia hii ni alama sahihi ya kunifanya kuongeza bidii,kujituma na kuendeleza hapa nilipofikia,"amesema Okuly

Pia Okuly ameongeza kuwa Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia inafanya kazi kubwa sana kuhakikisha Taifa linajikomboa kifikra na kuzalisha taifa lenye Ujuzi na maarifa ya kutosha katika kuleta Majawabu na masuluhisho ya changamoto mbalimbali zinazoikahili jamii.

No comments:

Post a Comment