BASHE NA MUSUSA WAKUTANA KUJADILI UWEKEZAJI KATIKA ZAO LA SHAYIRI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Tuesday, March 28, 2023

BASHE NA MUSUSA WAKUTANA KUJADILI UWEKEZAJI KATIKA ZAO LA SHAYIRI



Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Husein Mohamed Bashe amefanya kikao na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi Tanzania Breweries limited ( TBL) Ndg Leonard Mususa akiambatana na Ndg John Blood , Afisa Mkuu wa Ushirikiano Ndg Andrew Whiting, Makamu Mwenyekiti wa TBL Bi. Mesiya Mwangoka, Mkurugenzi Masuala ya Afrika, Kwa Pamoja wamejadiliana kuhusiana na uwekezaji wao katika zao la Shayiri

Katika Majadiliano hayo , Waziri Bashe amepokea taarifa ya utekelezaji wa Makubaliano yaliyofanyika Mwaka Jana wa kufufua kiwanda cha Shayiri kilichopo Mkoa wa Kilimanjaro, Ikiwa ni Makengo ya kufikia kutoagiza Shayiri kutoka Nje ya Nchi baada ya Mwaka Mmoja.


Aidha Wizara na TBL wamekubaliana kuzalisha Shayiri kupitia mradi wa Vijana na wanawake wa BBT na Ushiriki wao katika Block Farms system.

Vilevile Waziri Bashe amepokea Taarifa ya mfumo mpya wa kuhudumia wakulima kwa kutumia technolojia ya kisasa ( Block chain Farming System) Mfumo ambao umeshafanyiwa Majaribio Mwaka huu na kufanya Vizuri

Pia Wizara ya Kilimo itashirikiana na TBL kwenye Upande wa ICT, na kufanya kazi kwa karibu na TFRA kwa kutumia mfumo wa Block chain System katika Usambazaji wa Mbolea kwa Wakulima.

No comments:

Post a Comment