Na.Elimu ya Afya kwa Umma
Elimu ya ugonjwa wa Surua pamoja na uhamasishaji wa chanjo kwa njia ya magari ya matangazo na sinema imeendelea kuzaa matunda baada ya zaidi ya wananchi 200 kutoka kijiji cha Migunga kujitokeza kufuatilia kupata elimu hiyo usiku wa Machi 8.2023.
Hatua hiyo ni kutokana na Wizara ya Afya, Idara ya Kinga, Elimu ya Afya kwa Umma kuweka mkazo wa kuhakikisha kila mwananchi anakuwa na uelewa juu ya Surua na umuhimu wa kuwapeleka watoto chanjo.
Hivyo, pamekuwa na mwitikio mkubwa wa wananchi kuleta watoto wao kupatiwa chanjo baada ya kupata elimu hiyo ambapo wamekuwa wakiwaleta watoto kupata chanjo huku wakitazama sinema.
No comments:
Post a Comment