KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA MIRADI YA ASA ARUSHA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Thursday, October 5, 2023

KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA MIRADI YA ASA ARUSHA


Na Imma Msumba ; 

Arusha

Kamati ya kudumu ya Bunge

 ya Viwanda,Biashara ,Kilimo

na Mifugo imetembelea 

mradi wa ujenzi wa bwawa 

la umwagiliaji katika 

shamba la wakala wa 

mbegu za kilimo ASA katika 

eneo la Ngaramtoni ambapo 

kamati hiyo ilikuwa 

ikiongozwa na Mwenyekiti 

wa Kamati hiyo 

Mhe.Mariam Ditopile 

ambaye ni Mbunge wa Viti  

Maalum kupitia Mkoa wa 

Dodoma.


Akizungumza katika ziara 

hiyo kwa niaba ya 

mwenyekiti wa kamati hiyo 

Ezra Chiwaleza ambaye ni 

Mbunge wa Biharamulo 

amesema wanampongeza 

sana Rais wa Jamuhuri ya 

Muungano wa Tanzania 

Samia Suluhu Hassan kwa 

kazi kubwa aliyoifanya na 

kutoa pesa nyingi 

anazoendelea kuwapatia 

katika wizara ya kilimo 


“kama tulivyoona mradi 

huu wa ASA uliopo 

Ngaramtoni kazi 

inayoendelea ni kubwa 

bwawa limechimbwa na liko 

katika hali nzuri na kufikia 

katika hatua ya umaliaziaji .


“Pia tumpongeze 

mkandarasi anayefanya kazi 

hii kazi inaridhisha kama 

kamati tumefika hapa 

tumeona kazi ni nzuri na 

tunampongeza pia 

mkurugenzi kwa kazi 

kubwa anayoifanya “alisema


Kikubwa sisi tumewahasa 

kwa yale ambayo wanaona 

kwamba wanayaitaji kama 

kamati ilikuweza kuifikia 

 ndoto ya Rais kwenye 

kuwahudumia watanzania 

wayalete kazi ya kamati  

tunapokuja hapa hatuji 

kama mahakimu tunakuja 

kuona changamoto ambazo 

wanazo watendaji hususani 

taasisi ambazo ziko chini ya 

wizara ili twende tukaseme 

kwa niaba yao kama kamati 

inayosimamia wizara hizi ili 

pesa inayoitajika iweze 

kupatikana kwaajili ya 

kufanya utekelezaji.


Kamati imeridhika na 

miradi inayoendelea hapa 

miradi ni mizuri tunazidi 

kuwauunga mkono kwahiyo 

wafanye haraka kwa wale 

ambao wanayo ili kamati hii 

chini ya mwenyekiti wetu 

tuone ni jinsi gani 

tukashauri serikali ili  yale 

ambayo yanaitajika kwaajili 

yakuweza kuongezea nguvu  

yaongezewe nguvu ili  

waweze kuwahudumia 

watanzania maana  kazi 

inayofanywa na ASA ni 

kuhakikisha watanzania 

wanapata mbegu bora 

ilipale unapolima eneo dogo 

uweze kuzalisha kwa wingi.       


 “Sasa kama kazi hii 

haitafanyika  maana yake 

watanzania wataumia 

watakuwa wanatumia 

mbegu zilezile za kienyeji 

unalima hekari ishirini 

unavuna kidogo ila 

aliyelima hekari tano 

anavuna zaidi yako 

wewe”aliongezea



 Naye Naibu waziri wa 

kilimo Ernest Silinde 

ameeleza kuwa wizara 

inafanya kazi kwa karibu na 

kamati hiyo na inajukumu 

la kupitisha fedha na moja 

ya jukumu lao ni kuangalia 

maendeleo ya mradi na 

kushauri kwa kutoa 

mapendekezo kulingana na 

kile walichokiona.


“Niwahakikishie kamati ya 

bunge kwamba maoni yao 

ushauri wao wote walioutoa 

sisi kama wizara 

tumeyapokea 

na tutakwenda 

kuyafanyia kazi kama 

ambavyo tumekuwa 

tukifanya hivyo mara kwa 

mara”


Hata hivyo nipende 

kuwaeleza watanzania 

mashamba haya ni kazi 

nzuri inayofanywa na Dkt. 

Samia hayani maono yake ni 

maoni ya Ilani ya chama cha 

mapinduzi maono haya 

yanayofanyika hapa 

yamekusudia jambo moja 

kuongeza uzalishaji wa 

mbegu bora hapa nchini 

kwasababu tunahitaji 

mbegu bora na zauhakika 

katika muda wote wa 

msimu.


"Tumekuwa na changamoto 

ya mbegu kwa muda mrefu 

tumekuwa tukitumia fedha 

za kigeni kuagiza mbegu 

nchini kwahiyo tukiongeza 

uzalishaji maana yake 

tutapunguza matumizi ya 

fedha za kigeni nje ya nchi 

mpaka kufikia 2030 tuwe 

tumeondoa uhaba wa mbegu nchini." Aliongezea


Kwaupande wake Mkuu wa 

Mkoa wa Arusha John 

Mongella,ameiomba kamati 

hiyo kuhakikisha mashamba 

11 yawawekezaji 

yaliyorudishwa serikalini 

takribani miaka mitano 

iliyopita wayafanyie 

mpango 

iliyaweze kurudi katika 

wizara ya kilimo ili 

yakaendelezwe kwani soko 

la dunia ya sasa linataka 

mbogamboga na maua 


“mwenyekiti wa kamati 

shamba moja lilikuwa 

linaajiri zaidi ya 

wafanyakazi elfu moja 

asilimia 90 ya wafanyakazi 

hao walikuwa ni wanawake 

na vijana ”alisema

 

No comments:

Post a Comment