KAMATI YA SIASA YA CCM KATA YA KILIMANI YAKAGUA MRADI WA UJENZI WA SHULE. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, October 11, 2023

KAMATI YA SIASA YA CCM KATA YA KILIMANI YAKAGUA MRADI WA UJENZI WA SHULE.


Na Barnabas Kisengi -Dodoma

Viongozi wa Kamati ya Siasa ya Kata ya Kilimani Jijini Dodoma pamoja na Wajumbe wa Sekretarieti ya kata ya Kilimani Wamefanya ziara yakukagua Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Msingi unaotekelezwa katika Mtaa wa chinyoyo kata ya Kilimani na kuridhishwa na utekelezaji wake.

Pamoja na kuona kasi ya ujenzi huo unavyoendelea viongozi hao wamesisitiza ujenzi huo uongezewe kasi ili ukamilike kwa haraka.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Kilimani Nathani Chibeye amesema ujenzi huo wa shule ya msingi utakuwa mkombozi kwa kata ya kilimani.


"Kwa kuwa Kata hii tangu ipate Uhuru haijawahi kuwa na shule ya msingi jambo ambalo hupelekea watoto wa mitaa nne ya Kilimani kusoma katika shule za kata nyingine na kusababisha kutembea umbali mrefu kuitafuta elimu.,"Amesema

Licha ya hayo amesema wao kama viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Kilimani wanaishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwapatia fedha za ujenzi wa shule hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwa wananchi wa kata ya Kilimani.


Kwa upande wake Katibu wa Chama hicho Kata ya Kilimani Rotta Ndimbo ameitaka kamati ya ujenzi na mkandarasi kuhakikisha wanatanguliza uzalendo katika ujenzi wa shule hiyo ili thamani ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi huo zinatumika kama zilivyo kusudiwa.

Ziara hiyo ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Kilimani ni mwendelezo wa kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali katika kata ya Kilimani ili kuhakikisha utekelezaji wa ilani ya chama unafanikiwa.

No comments:

Post a Comment