TRA : UINGIZAJI WA BIDHAA KWA NJIA ZA MAGENDO NI HATARI KWA AFYA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, October 25, 2023

TRA : UINGIZAJI WA BIDHAA KWA NJIA ZA MAGENDO NI HATARI KWA AFYA

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi, kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Richard Kayombo amesema uingizaji bidhaa kwa njia ya magendo sio tu kwamba unapoteza mapato ya serikali bali pia ni hatari kwa afya za watumiaji.

Bw. Kayombo ameyasema hayo wakati akijibu swali, nini madhara yanayotokana na uingizwaji wa bidhaa za magendo nchini, kwenye kipindi cha maswali na majadiliano katika Kongamano la Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano wa Taasisi za Wizara ya Fedha na Wahariri wa Vyombo vya Habari, mjini Morogoro Oktoba 25, 2023.

“Kuna madhara ya kukosa kodi, lakini uingizwaji wa bidhaa za magendo baadhi ni hatari kwa afya za binadamu, zinaingizwa bila ya kupitia kwenye vyombo vya udhibiti ubora.” Alisema.

Alitoa mfano kule Wilayani Kilwa, Mkoa wa Lindi, ambako TRA, ilikamata sukari ikiwa kwenye vifungashio vya viwanda vinavyotambulika nchini, lakini mazingira ya eneo lililokuwa likitumika kufungashia sukari hiyo halikuwa zuri kiafya,” alisema na kuongeza..pia tulikamata mafuta ya kula, kuna mengine tuliyamwaga baada ya Mamlaka ya Udhibiti Ubora, kuthibitisha kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu.” Alifafanua Bw. Kayombo.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi, kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Richard Kayombo, akitoa wasilisho lake kuhusu utekelezaji wa majukumu TRA
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, anayeshughulikia Huduma za Hazina, Bi. Jenifa Christian Omolo, akipena mikono na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Richard Kayombo.
Baadhi ya Washiriki wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi, wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.
Baadhi ya Washiriki wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi, wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.


Bi. Scola Malinga, kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha

No comments:

Post a Comment