MABADILIKO YA SHERIA YA PPP KUMLINDA MWEKEZAJI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, October 25, 2023

MABADILIKO YA SHERIA YA PPP KUMLINDA MWEKEZAJI

 

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO

KAMISHNA Msaidizi idara ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), Wizara ya Fedha, Bw. Bashiru Taratibu, amesema, mabadiliko ya sheria ya ubia kati ya serikali na sekta binafsi yamelenga kumlinda mwekezaji.

Amesma hayo wakati akiwasilisha mada ya Sheria ya PPP, mwishoni mwa kongamano la siku mbili la wasimamizi wa mitandao ya kijamii (Online Media) na Wizara ya Fedha mjini Morogoro, Oktoba 24, 2023.

Amesema huko nyuma sheria haikuwa rafiki kuwezesha utekelezaji wa miradi kwa njia ya ubia PPP.

“Ni matarajio ya serrikali, kuwa baada ya marekebisho ya sheria ya PPP Sura ya 103 ya mwaka 2023 kuidhinishwa na Rais, ile miradi ya PPP zaidi ya 60, ambayo imeandaliwa na pande zote mbili serikali na sekta binafsi, sasa itakwenda kutekelezeka kwa manufaa ya pande zote.” Alisema.

Alisema kabla ya sheria, moja ya vikwazo ilikuwa ni mamlaka za serikali, ambapo walichukua hadi mwaka mzima kujadiliana kabla ya kufikia uamuzi, lakini mabadiliko ya sheria hii yanaelekeza kuwa kila baada ya miezi mitatu itolewe taarifa ya hatua iliyofikiwa ili uamuzi ufikiwe.

“Sheria ya sasa inatamka ununuzi wa mbia ufanyike kwa uwazi na ushindani ili kumpata mtu sahihi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.” Alisisitiza Bw. Taratibu na kuongeza..

“Tunaenda kwenye sekta binafsi ili kupata vitu vitatu ambavyo ni pamoja na kupata fedha ya kutekeleza mradi, ujuzi wa uendeshaji ambao serikali haina, pia teknolojia.” Alifafanua.

Aidha, Sheria hii ya sasa inatamka kuwa Mbia lazima awe amesajili kampuni yake kwa mujibu wa sheria ya makampuni ya Tanzania.

Alisema baadhi ya miradi ya PPP ambayo ‘imeiva’ ni pamoja na mradi wa ujenzi wa barabara ya njia nne kila upande, Kibaha-Chalinze awamu ya kwanza na Chalinze- Morogoro.

KAMISHNA Msaidizi idara ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), Wizara ya Fedha, Bw. Bashiru Taratibu

 

Mwenyekiti wa washiriki, Bw. Mathias Canal, akizungumza wakati wa kufunga kongamano hilo

Kamishna Msaidizi idara ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), Wizara ya Fedha, Bw. Bashiru Taratibu (katikati) akijadiliana jambo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja (kulia) na Afisa Tawala Wizara ya Fedha, Bw. Bw. Brighton Ngowo

Baadhi ya washiriki

Kamishna Msaidizi PPP, Bw. Taratibu
Mhasibu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, CPA.  Jenipha J. Ntangeki

Mhariri wa Maudhui Mtandaoni, kutoka Mwananchi Communications, Bw. Muyonga Jumanne (kushoto) akichangia wakati wa majadiliano. Kulia ni Mmiliki wa Okuly Blog, Bw. Okuly Julius.

Issa Lazaro, Mkuu wa Digital, Wasafi media, akizungumza kwenye kongamano hilo.

No comments:

Post a Comment