 |
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi akizungumza wakati wa kikao cha kupokea mfano wa ratiba ya viongozi katika mfumo wa kielektroniki kutoka kwa Mamlaka ya Serikali Mtando (eGA) kilichofanyika katika Ukumbi wa ofisi hiyo Tarehe 21 Novemba 2023 Jijini Dodoma. |
 |
Mkurugenzi wa Tafiti kutoka Mamlaka ya Serikali Mtando (eGA) Dkt. Jaha Mvulla (aliyesimama) akiwasilisha Mfano wa ratiba ya viongozi ya kielektroniki kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi pamoja na wataalam kilichofanyika katika Ukumbi wa ofisi hiyo Tarehe 21 Novemba 2023 Jijini Dodoma. |
 |
Baadhi ya Wataalam kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakisikiliza kikao akilichofanyika kwa lengo la kuwasilisha Mfano wa ratiba ya viongozi ya kielektroniki kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi kilichofanyika katika Ukumbi wa ofisi hiyo Tarehe 21 Novemba 2023 Jijini Dodoma. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU) |
Na Mwandishi wetu – Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amepokea wasilisho la mfano wa ratiba ya viongozi katika mfumo wa kielektroniki kutoka kwa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA).
Mfumo huo wa kielektroniki utasaidia viongozi kufahamu ratiba zao za utekelezaji wa majukumu ya kila siku katika mfumo ikiwa ni pamoja na kusoma taarifa, kutoa maoni na maelekezo katika eneo la kazi na uratibu wa shughuli za ndani za wizara husika.
Imeelezwa kuwa mfumo huo utawezesha viongozi kujipanga katika majukumu ya kila siku na kuondoa mgongano wa ratiba zao katika ngazi zote.
Ofisi ya Waziri Mkuu iliandaa kikao kazi na wataalam kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao eGA kwa ajili ya kuwezesha moduli hii ya kalenda ndani ya mfumo wa DASHBOARD ambapo mpango kazi huo unaonesha muda ambao eGA watatumia kukamilisha kalenda hiyo pamoja na muda wa kuanza kutumika rasmi.
No comments:
Post a Comment