WAZIRI CHANA AHIMIZA USHIRIKIANO KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Wednesday, December 6, 2023

WAZIRI CHANA AHIMIZA USHIRIKIANO KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA

Na Okuly Julius - Dodoma

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Balozi Pindi Chana ametoa wito kwa taasisi na vyombo vya Serikali, mashirika ya kiraia,ya wanawake, vijana, sekta binafsi, vyombo vya habari, na mfumo wa Umoja wa Mataifa kuungana ili kukabiliana na ukatili dhidi ya wanawake na wasichana kwa wigo wa kimataifa.


Balozi Chana ametoa wito huo leo Disemba 6,2023 jijini Dodoma, wakati akizindua muendelezo wa shughuli ya Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mkoa wa Dodoma.


Akitoa wito huo,Balozi Chana amewaomba wadau wa Maendeleo kuongeza juhudi za pamoja kuzuia ya ukatili kwa wanawake na wasichana


‘‘ Niwaombe muongeze mashirikiano ya muda mrefu na usaidizi kwa kuunga mkono juhudi za Serikali kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia miongoni mwa jamii,’’ alisisita waziri Chana.


Sambamba na hilo akawakumbusha wadau wa maswala ya jinsia kushiriki mapambano hayo hasa kwa watu wasiofikiwa .


“Kwa mashirika yanayotetea haki za wanawake na Watoto, niwaombe tujikite zaidi katika maeneo ya pembezoni kwani kule ndipo kwenye changamoto zaidi. Na hii inatokana na ukweli kwamba, elimu ya masuala haya bado haijafika vya kutosha kwahiyo jamii bado inaamini katika mila na desturi,’’ aliongeza waziri huyo


Aidha atumia fulsa hiyo kuwakumbusha watendajiwa serikali kuendelea kutoa ushirikiano kwa wadau wote kwenye mapambano hayo.


“niwasihi muendelee kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa Mama Samia Legal Aid Campaign ikiwa ni mojawapo ya mkakati madhubuti wa kuelimisha jamii kuhusu kuzuia na kukabiliana na ukatili wa kijinsia hapa nchini hususan kwa wanawake na watoto,”alikumbusha Balozi Chana


Sambamaba na hilo, amezitaka Taasisi za umma, kuendelea kuwajengea uwezo wanawake na wasichana kwa kuwashirikisha kwenye nafasi mbalimbali za siasa, utungaji sera, na uamuzi kutoka ngazi kijiji au mitaa, taifa za kimataifa.


Kwa upande wa wananchi amewakumbusha kushirikiana na viongozi wa Serikali za mitaa na Serikali Kuu, kuimarisha ulinzi ili kuzuia               na kuondoa tabia za ukatili, unyanyasaji, vitisho na ubaguzi dhidi ya wanawake, watoto na watetezi wa haki za binadamu.


Kwa upande wa  vyuo vya taalamu Waziri huyo amewataka kutumia  vyema dhamana waliyopewa katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya kazi ,kwa kupiga vita  rushwa au upendeleo unaosababisha ukatili wa kinjisia  kwa wanawake na wasichana wawapo chuoni.


Akizungumza kwa niaba ya  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM)  Prof.Albino Tenge amesema kuwa chuo hicho kinaendelea kuwajenga vijana katika misingi ya kuwa mabalozi wema wa kupamabana na  masuala ya ukatili wa kijinsia na kuwapa nafasi ya kushiriki kampeni mbalimbali ikiwa ni kwa njia ya kwenda kutoa elimu kwa jamii au kushiriki midahalo mbalimbali Sio tu katika siku hizi 16. 


“Tunaweza tu kusonga mbele na kuushinda Ukatili wa Kijinsia ikiwa tutazungumza na kupaza sauti. Hivyo sisi  Chuo Kikuu Cha Dodoma kwa pamoja wote tunasema, Unyanyasaji wa kijinsia hauna nafasi katika nchi hii. Sio tu katika siku hizi 16, bali iwe katika maisha yetu ya kila siku. Kila mmoja wetu ajitathimini ni kwa kiasi gani anachangia kuzuia vitendo vya ukatili wa kijinsia katika familia yake, eneo lake la kazi na jamii kwa ujumla, Na kisha achukue hatua,”amesema Prof. Tenge.

 

Hadi sasa jumla ya madawati 1,850 ya jinsia yameanzishwa kati ya hayo 1,128 kwenye shule za msingi na 772 shule za Sekondari.


Kwa upande wa Taasisi za elimu za juu hadi sasa jumla ya madawati 273  yameanzishwa likiwemo dawati la Chuo Kikuu cha Dodoma  na kufanya idadi hiyo kufikia asilimia 44 ya  lengo la kuwa na madawati 612 ifikapo mwezi Juni 2024.




No comments:

Post a Comment