ERB NA CRB WATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI BASHUNGWA,WATOA RIPOTI UCHUNGUZI WA AJALI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Thursday, February 8, 2024

ERB NA CRB WATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI BASHUNGWA,WATOA RIPOTI UCHUNGUZI WA AJALI

Msajili wa Bodi ya Wahandisi (ERB) Mhandisi Benard Kavishe ,akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 8,2024 Jijini Dodoma na kutoa taarifa  ya uchunguzi wa ajali ya kuvunjika kwa Kalavati katika barabara ya Kanyinabushwa Mbale “A” iliyoko Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera

Msajili wa Bodi ya Makandarasi (CRB)Mhandisi Rhoben Nkori ,akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 8,2024 Jijini Dodoma na kutoa taarifa  ya uchunguzi wa ajali ya kuvunjika kwa Kalavati katika barabara ya Kanyinabushwa Mbale “A” iliyoko Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera.




Na Okuly Julius ,DODOMA


Kufuatia maeelekezo yaliyotolewa na  Waziri wa Ujenzi Innoncent Bashungwa mnamo Januari 17,2024 baada ya ajali ya kuvunjika kwa Kalavati katika barabara ya Kanyinabushwa Mbale “A” iliyoko Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera, Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) Pamoja na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) zimetoa taarifa za uchunguzi wa ajali hiyo na kumtaka mkandarasi kurudia ujenzi wa Kalvati hilo kwa gharama zake.

 

Taarifa hiyo imetolewa leo Februari 8,2024 Jijini Dodoma na Msajili wa Bodi ya Wahandisi Mhandisi Benard Kavishe mbele ya wanahabari na kuongeza kuwa mapungufu yaliyosababisha uharibifu huo yalisababishwa na mkandarasi hivyo wamemchukulia hatua stahiki kwa mujibu wa sharia ya Usajili wa Wakandarasi sura ya 35 ya mwaka 2002.


“ERB na CRB ziliunda timu ya Wataalamu kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa ajali hiyo ambapo timu ilichukua hatua ya kutembelea mradi huo Jnauari 20,2024, kufanya mahojiano na TARURA mkoa wa Kagera,Msimamizi wa mradi na mkandarasi,kupitia nyaraka za mradi huo na kuandaa ripoti ya uchunguzi iliyobainisha chanzo cha kubomoka kwa daraja dogo na kupendekeza hatua stahiki” amesema Mhandisi Kavishe


Ambapo Mhandisi Kavishe amebainisha matokeo ya uchunguzi huo kuwa ni kutozingatiwa kwa matakwa ya mkataba ,hasa uwepo wa wataalamu walioainishwa, kutumika kwa malighafi hafifu kinyume na matakwa ya mkataba na kuruhusu kupita kwa vyombo vya moto kabala ya Kalvati kukamilika ujenzi wake.


Kwa upande wake Msajili wa Bodi ya Makandarasi Mhandisi Rhoben Nkori amewataka wadau wa sekta ya ujenzi kwa ujumla kuzingatia Sheria ,Kanuni na Miongozo katika utekelezaji wa miradi.


Ikumbukwe kuwa Mkandarasi EACI Company Ltd ndio alikuwa anatekeleza ujenzi wa mradi huo ambapo tayari ameshachukuliwa hatua za kisheria na Bodi  zote mbili ikiwemo kutakiwa kurudia ujenzi wa mradi huo kwa gharama zake mwenyewe ili wananchi waanze kutumia Kalvati hiyo kw utekelezaji wa shughuli zao za kila siku.

No comments:

Post a Comment