Akitoa taarifa leo tarehe 25 Machi 2024 Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa jitihada kubwa zinaendelea za kurudisha mawasiliano ya barabara katika eneo hilo.
“Timu za TANROADS kutoka Mikoa ya Lindi na Pwani zimeungana kuongeza nguvu ili kabla ya mchana safari ziweze kuendelea. Tunawapa pole wasafiri wote kwa changamoto iliyojitokeza”, ameeleza Waziri Bashungwa.
Kwa upande wao Meneja wa TANROADS wa Mikoa ya Lindi na Pwani Mha. Emil Zengo na Mha. Baraka J. Mwambage wamesema wanafanya kila jitihada kurejesha mawasiliano ya barabara hiyo haraka ili ili Wananchi waweze kuendelea na shughuli zao za uzalishaji.
No comments:
Post a Comment