AMAMA FARMS LTD MBANGUAJI BORA WA KOROSHO KWA MWAKA 2023/ 2024. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Monday, August 26, 2024

AMAMA FARMS LTD MBANGUAJI BORA WA KOROSHO KWA MWAKA 2023/ 2024.




Na Carlos Claudio, Dodoma.


Amama Farms Limited yaibuka na tuzo ya mbaguaji bora wa korosho katika kundi la wabanguaji wakubwa wa korosho kwa mwaka 2023/ 2024.


Tuzo hiyo imetolewa katika mkutano  Mkuu wa Wadau wa Tasnia ya Korosho wa siku mbili ulioanza Julai 22, 2024  na kutamatika Julai 23, 2024 jijini Dodoma.

Mkutano huo mkuu ulitamatika kwa mjadala wa pamoja ukifuatiwa na tuzo mbali mbali zilizotolewa ambapo Amama Farms Limited iliibuka kidedea kwa kunyakua tuzo ya kundi bora la mbanguaji mkubwa wa korosho kwa msimu wa mwaka huu.


Kiwanda cha Amama kilianza shughuli (kuanzisha tena kiwanda) mnamo mwaka 2022, kikiwa na lengo la kuongeza thamani ya mazao ya chakula ya ndani na kubadilisha kilimo cha Tanzania kutoka kuwa muuzaji wa malighafi yenye thamani ya chini hadi kuwa sekta ya mauzo ya nje ya bidhaa zilizosindikwa zenye ubora wa juu.


Kiwanda hicho kinapatikana Tandahimba, mji mdogo Kusini mwa Tanzania karibu na mpaka wa Msumbiji ikiwa ni kiwanda pekee cha kubangua korosho katika eneo hilo, sehemu ya kipekee kwa kubadilishana ujuzi, taarifa, msaada na matumaini ya siku za usoni.


Akipokea tuzo hiyo katika hitimisho la mkutano huo Bwn. Willem Warmenhoven amesema, “ ni furaha kwangu pamoja na familia ya Amama Farms Ltd, tuzo hii sio kwa Amama tu, ni kwa niaba ya wabanguaji wote humu, kwani tuzo hii ni chachu ya uchapaji kazi na mimi sipaswi kuzungumza yote haya lakini tunaishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani wamekuwa msaada mkubwa katika kutoa ushauri na kushirikiana na kampuni za korosho”.



Warmenhoven hakuficha kusema kuwa Korosho za Tanzania ni moja ya zao bora kulinganisha na za nchi nyengine kwani zina ladha tamu na kubwa , pia ameeleza kuwa mabadiliko ya hali ya hewa ni moja ya changamoto wanazokumbana nazo katika zao hilo la korosho.


Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji Hussein Bashe akiwa mgeni rasmi katika mkutano huo mkuu amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kuwaweka ndani na kuwafungulia mashitaka viongozi wa Vyama vikuu vya ushirika na Viongozi wa maghala ambao wanajihusisha na uhujumu wa zao la korosho nchini.


Waziri Bashe amewaambia wajumbe wa mkutano huo, “nilipata aibu pale nilipopokea mgeni kutoka nchini India, ambaye alinifuata bungeni wakati wa vikao vya Bajeti akinilalamikia kwamba ameuziwa Korosho kutoka Tanzania ambazo hazifai zimebadilika hata rangi, kama zao hilo mtaendelea kulifanya hivyo huenda mkaliua siku si nyingi, sitakubali watu wachache waliue zao hili hivyo mimi na wao mpaka kieleweke”.

Tuzo ya mbaguaji bora wa korosho katika kundi la wabanguaji wakubwa wa korosho kwa mwaka 2023/ 2024.


Baadhi ya wakuu wa Mikoa inayolima zao la korosho wakiwa katika mkutano huo.

1 comment:

  1. Nice to meet you.

    I am CEO of KoA PRECIOUS Co.,Ltd in South Korea(Mr.Sung)

    I want to import huge quantity cassava Starch powder(tapioca) from your country.

    I send you details as below
    =======================
    ** I explain detailed procedure and payment terms and quantity and specifications as below.

    (China buyer company is big factory for ethanol production with cassava Starch(Tapioca)
    1)Seller company send FCO and chemical report to me.

    2) After the China buyer check the chemical report, the China buyer send an ICPO to Seller company.(TT payment)

    3) After that, China buyer company and Seller company make SPA(contract document) directly.

    4) Seller company move the product to shipping port of seller company.

    5) China buyer travels to shipping port and make all the export process
    with Seller company.
    (Chinese inspector will be dispatched at shipping port to control monthly shipping continuously
    for 1 year over for contract duration)

    6) China buyer pays TT.90% of the Invoice after checking everything in departure port of seller company
    before shipping.

    7) China buyer pays TT.10% balance after the product reaches the destination(China, Guangxi qinzhou Port)
    ====================
    And also. Below payment terms are possible.

    NON-Transfer LC / irrevocable L/C
    ====================
    **Price: CIF, US$250/ton. China

    Destination)China guangxi qinzhou Port
    ================
    **About quantity as below

    1) 1st trial: 56ton(40ft container×2each) for quarantine test
    (Especially,Seller company can reconfirm mutual trust about China buyer company through 1st trial )

    2) Next step: minimum 2,000ton/every month, maximum 50,000ton over/ every month
    (You can increase the monthly quantity step by step)
    ==================
    **About product purpose and specifications and test standards as below

    1)My china buyer purpose of cassava starch powder is for ethanol production. Not for food.

    2)So, the starch ratio needs to be at least 86%.

    3) Quality Test standard as below

    3-1) Buyer quality test standard (Starch contents: Min86%, Moisture: Max 12%, Ph: 5~7)

    3-2) Quarantine quality test standard (Spot: Max 3 each/cm², Sulfur dioxide residual amount: Max 0.03g/kg)
    =====================
    My whatsapp phone number is +82-10-7653-6226(Mr.Sung)

    If you can make supply chain about cassava starch, you can get commission and shipping fee at the same time, stably and continuously.
    If you want, you can contact my general manager in Gabon and my managers in Kenya, Tanzania, Ghana, Nigeria, Sierra Leone, South Africa.
    I will wait for your answer

    Thank you

    ReplyDelete