
NA. MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwan Kikwete ametembelea banda la Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) katika maonesho ya Wiki ya Wanawake yanayoendelea viwanja vya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.
Kilele cha Siku ya Wanawake Duniani ni tarehe 8 Machi ya kila mwaka ambapo Kitaifa yanaadhimishwa mkoani humo yenye kauli mbiu isemayo; "Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji"
Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.





No comments:
Post a Comment