Dar es Salaam, 19 Mei 2025 – Equity Group, chini ya Mpango wa Afrika wa Urejeshaji na Uhimilivu (ARRP), inaongoza msafara wa kimataifa wa biashara na uwekezaji katika Afrika Mashariki, ukiaanzia nchini Tanzania (Dar es Salaam na Zanzibar) na kuendelea Uganda (Kampala). Msafara huu unalenga kuangazia fursa za kiuchumi na kukuza ushirikiano wa kikanda.
Msafara huo wa wiki moja umeandaliwa kwa kushirikiana na Equity Bank Tanzania na Equity Bank Uganda, ukiwavuta zaidi ya wawekezaji 200 kutoka nchi 15, pamoja na wajasiriamali, makampuni ya uwekezaji, na wadau wa maendeleo ili kukuza uwekezaji wa mipakani kwa kushirikisha sekta muhimu kama Kilimo-biashara, Nishati mbadala, Utalii na hoteli, Madini na miundombinu pamoja na Uchumi wa Buluu (Blue Economy) kuchangia uundaji wa ajira na ukuaji wa uchumi wa jumuishi.

Akizungumza katika kongamano la Maonesho ya Biashara na Uwekezani (Equity Trade and Investment Roadshow 2025) ameiopongeza Benki ya Equity kwa kuwaleta pamoja wawekezaji wa ndani na wa kimataifa, wajasiriamali na washirika wa maendeleo na kusema kuwa hiyo sehemu ya utekelezaji wa mpango wa ARRP chini ya nguzo ya Biashara na Uwekezaji, kwa lengo la kukuza uchumi jumuishi na shindani kikanda.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Bank Tanzania, Isabela Maganga amesema Msafara huu ni jukwaa la kuiweka Tanzania kama kiungo muhimu katika mnyororo wa thamani kikanda na kimataifa, unatoa fursa ya kipekee kwa wawekezaji wa kimkakati kwenye masoko ya kikanda na uwezo mkubwa katika sekta mbalimbali na ni jukwaa la kuiweka Tanzania kama kiungo muhimu katika usambazaji wa kikanda na kimataifa.
"Tanzania ina masoko makubwa, idadi ya watu inayokua, na rasilimali kwa sekta mbalimbali. Hii ni fursa ya kipekee kwa wawekezaji." alisema.

Msafara huu unafuatia mafanikio ya misafara mingine ya awali iliyosaidia uwekezaji wa mabilioni ya dola, katika nchi mbalimbali ikiwa ni pamoja na:
Kenya–DRC
Marekani–Tanzania
India–Rwanda–Uganda
Singapore–Kenya
Athari ya Mpango wa ARRP
Kwa kusudi la kufikia watu na biashara milioni 100 ifikapo 2030. Equity Group inatarajia kurejesha asilimia 2 ya pato la taifa Afrika Mashariki kwenye sekta binafsi na kuunda ajira milioni 50 barani Afrika.
Msafara huu unaonesha jitihada za Equity Group kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kuvumbua fursa kwa wawekezaji kimataifa. Kwa kushirikiana na serikali na sekta binafsi, Afrika Mashariki inaweza kuwa kivutio kikuu cha uwekezaji na ustawi wa kijamii.

Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Bank Tanzania, Isabela Maganga akiteta jambo na Mkuu wa Chuo Cha Elimu ya Biashara (CBE) Prof. Edda Tandi Lwoga wakati wa kongamano la Maonesho ya Biashara na Uwekezani (Equity Trade and Investment Roadshow 2025) , lililoandaliwa na Benki ya Equity Tanzania na kufanyika jijini Dar es salaam leo.
.jpg)
Mkurugenzi wa Biashara wa Equity Bank Tanzania, Prosper Nambaya akizungumza wakari alipokuwa akiwasilisha mada yake katika kongamano la biashara na uwekezaji katika Afrika Mashariki, lililoandaliwa na Benki ya Equity Tanzania na kufanyika jijini Dar es salaam leo.

No comments:
Post a Comment