
Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) kwa Kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma wanatarajia kufanya Mkutano wa Kimataifa wa masuala ya huduma za Afya za upandikizaji wa viungo vya mwili (Organ Tranplants).
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa BMH Prof. Abel Makubi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Ugonjwa wa Selimundu Duniani yaliyofanyika katika Hospitali hiyo ambayo kwa sasa ndio pekee nchini Tanzania inayotoa huduma ya kutibu ugonjwa wa Selimundu kwa njia ya kupandikiza Uloto kwa watoto wenye ugonjwa huo.
Mkutano huo tunatarajia utafanyika mwakani, utahusisha Wataalamu wa Kitaifa na Kimataifa ili kusaidia kukuza na kubadilishana Uzoefu, ujuzi na utaalamu na kutoa fursa ya kutangaza uwekezaji na mapinduzi makubwa yaliyofanywa na Serikali katika sekta ya Afya" alifafanua Prof. Makubi.
No comments:
Post a Comment