Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa, leo Juni 9,2025 anatarajiwa kufungua rasmi mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi na Sekondari yanayofanyika Kitaifa Mkoani Iringa.
Ufunguzi huo utafanyika katika viwanja vya michezo Kichangani Manispaa ya Iringa, na kuhudhuriwa na wanamichezo zaidi ya 3,000 kutoka mikoa yote ya Tanzania, ambao tayari wameshawasili Mkoani humo.
Maandalizi ya zoezi hilo la ufunguzi yameshakamilika, likiwa lilitanguiiwa na ufunguzi wa Baraza la UMITASHUMTA lililofanyika jana tarehe 8 Juni 2025 katika viwanja vya shule ya Sekondari Lugalo-Iringa.
UMITASHUMTA & UMISSETA inaandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI ikishirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Utamaduni na Michezo.
Kauli mbiu ya Mashindano ya mwaka huu ni "Viongozi bora ni msingi wa maendeleo na Taaluma, Sanaa na Michezo,Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu"
No comments:
Post a Comment