
Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango akizungumza kwenye kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (kushoto kwake) wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Mifumo na Huduma za TEHAMA, Bw. Mohamed Mashaka.

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi. Mary Mwakapenda (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua jambo kuhusu TEHAMA wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Bw. Paul Seadin (aliyesimama) akichangia hoja wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua jambo kuhusu TEHAMA wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Sera za Tehama na Viwango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Ibrahim Toure (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam
Mradi wa Tanzania ya Kidijitali umeleta mapinduzi makubwa ya miundombinu ya TEHAMA nchini ikiwemo kuunganisha jumla ya taasisi za umma 600 ambazo ni Wizara, Mikoa, Halmashauri na Taasisi zote zilizohamia Dodoma ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi na watumishi wa umma.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.
“Mradi huu umeleta mafanikio makubwa katika kuunganisha Serikali kwenye mitandao ya TEHAMA ambapo taasisi 600 ikiwemo Wizara, Mikoa, Halmashauri na Taasisi zote zilizohamia Dodoma zimeunganishwa na mifumo ya TEHAMA ili kutoa huduma kwa wananchi na watumishi wa umma nchini, amesema Bw. Kiwango
Ameongeza kuwa katika kutoa huduma bora, watumishi wa umma wameendelea kutekeleza majukumu yao kupitia mifumo mbalimbali na kupimwa kupitia mifumo iliyojengwa ya Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma na Taasisi (e-Utendaji).
Aidha, Mfumo wa Daftari la Huduma za Serikali utawasaidia wananchi kupata huduma sehemu moja kwa urahisi, kwa wakati na kwa uwazi.
Mkurugenzi Kiwango ametoa wito kwa wananchi kutumia simu zao za viganjani kupiga namba *152*00# kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali za Serikali bila kufika katika ofisi husika endapo hawatakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.
No comments:
Post a Comment