PROF. ABEL MAKUBI AWAONGOZA MADAKTARI BINGWA WA BMH KUWAHUDUMIA WANANCHI WA BUJUMBURA - BURUNDI - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Monday, July 21, 2025

PROF. ABEL MAKUBI AWAONGOZA MADAKTARI BINGWA WA BMH KUWAHUDUMIA WANANCHI WA BUJUMBURA - BURUNDI


Na. Jeremiah Mbwambo, Bujumbura - Burundi


Mkurugenzi Mtendaji Prof. Abel Makubi leo ameongoza jopo la madaktari Bingwa wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kuwahudumuia wagonjwa waliofika katika kambi ya matibabu inayotolewa nchini Burundi katika Mkoa wa Bujumbura 

"Leo ni siku ya nane kuwepo hapa nchini Burundi, tulianzia mkoa wa Gitega na sasa tupo mkoa wa Bujumbura tumeona mwitikio ni mkubwa sana wa wananchi, mimi pamoja na madaktari tutawahudumia wananchi wote mpaka usiku" alisema Prof. Makubi 

Ameongeza kuwa wagonjwa wote tuliowafanyia upasuaji Gitega wanaendelea vizuri 

"Mtakumbuka tulifanya upasuaji wa wagonjwa 57 mkoani Gitega, wagonjwa wote wanaendelea vizuri na wengi wamesharuhusiwa kuendelea na shughuli zao" alisema Prof. Makubi. 

Hospitali ya Benjamin Mkapa imeendelea kujiimarisha katika matibabu ya tiba utalii katika ukanda wa Africa Mashariki, adhima ya Hospitali hii ni kutoa matibabu katika kiwango cha kimataifa.

No comments:

Post a Comment