Maelfu ya wananchi wa Lindi Mjini Mkoani Lindi leo Alhamisi Septemba 25, 2025 wakiwa wamejitokeza kwa wingi Kumlaki na kumsikiliza Mgombea wa Nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan, anayefanya Mkutano wake wa hadhara wa Kampeni katika Uwanja wa Ilulu, Lindi Mjini. Dkt. Samia yupo Mkoani Lindi tangu jana Septemba 24, 2025 na leo anatarajiwa kuhitimisha Mikutano yake Mkoani humo ya kuomba kura kwa wananchi na kueleza mafanikio yaliyopatikana kwenye serikali ya awamu ya sita.
Thursday, September 25, 2025
New
UWANJA WA ILULU LINDI MJINI WAFURIKA MAPOKEZI YA DKT. SAMIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment