Waziri Mkuu mstaafu Kassim Majaliwa ameonekana mapema leo asubuhi akiendesha baiskeli mitaa ya mbweni Jijini Dar es salaam, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kila siku wa kujenga afya na kuimarisha mwili.
Hatua hiyo imeendelea kutoa hamasa kwa Wananchi kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuboresha afya zao na kupunguza hatari ya magonjwa yasiyoambukiza.
Kwa mujibu wa Wataalamu wa Afya na Wadau wa Mazoezi, kuendesha baiskeli ni aina ya mazoezi ya mwili (cardio) ambayo husaidia kuimarisha moyo na mapafu, kuboresha mzunguko wa damu na kuongeza uwezo wa mwili kustahimili uchovu.




No comments:
Post a Comment