Na Boniphace John Epimack -Dodoma
Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imefanikiwa kufanya kwa mara ya kwanza upasuaji wa moyo kwa njia ya matundu kwa watoto watatu kutoka nchini Burundi ,hatua inayotajwa kuimarisha uwezo wa Tanzania katika kutoa huduma za kibingwa na kukuza utalii wa matibabu Barani Afrika.
Akieleza kuhusu mafanikio hayo leo Alhamisi ,julai 9,2026 hosiptalini hapo Jijini Dodoma ,Mkurugenzi mtendaji wa Hoslitali hiyo ,Profesa Abeli Makubi amesema Hatua hiyo inaendana na ajenda ya serikali ya kuendeleza utalii kwa kuvutia wagonjwa kutoka nchi jirani na mataifa mengine Duniani kupata huduma za kibingwa nchini Tanzania badala ya kusafiri nje ya afrika.
Profesa Makubi amesema Upasuaji huo wa watoto watatu kutoka Burundi umefanywa kwa ushirikiano kati ya wataalamu wa Hosipitali ya Benjamin Mkapa na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga uwezo wa ndani wa kutoa huduma za matibabu ya moyo nakupanua wigo wa huduma kwa wagonjwa kutoka nje ya nchi .
Ameongeza kuwa hapo awali huduma hiyo ilikuwa ikitolewa kwa watu wazima pekee ,lakini kutokana na kuimarika kwa uwezo wa hosipitali sasa imeanza kutolewa pia kwa watoto ambapo upasuaji huo umehusisha kuziba matundu ya moyo kwa watoto wa tatu ,huku watoto wengine waliopimwa
wakipatiwa matibabu mbadala baada ya kubainika kuwa hali zao hazikukidhi vigezo vya kitaalamu vya kufanyiwa upasuaji huo na kutokana na ukubwa wa athari za ugonjwa.
Aidha amesema kuwa kuimarika kwa huduma hizo kumepunguza idadi ya watanzania wanao lazimika kusafiri kwenda nje za nchi kufuata matibabu ya moyo.
Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka JKCI Godwin Sharao amesema utowaji huduma kwa wagonjwa wa kimataifa huwapa wataalamu fursa ya kubaini maeneo yanayo hitaji maboresho nakuongeza ushindani wa kitaaluma .
amesema kuhudumia wagonjwa kutoka mataifa mengine kutasaidia kutaendelea kuboresha ubora wa huduma za matibabu Tanzania.












No comments:
Post a Comment