MKURUGENZI WAMBUYA ATEMBELEA BANDA LA WMA NANE NANE - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Sunday, August 2, 2026

MKURUGENZI WAMBUYA ATEMBELEA BANDA LA WMA NANE NANE



Na WMA - DODOMA.


Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Needpeace Wambuya leo Agosti 2, 2026 ametembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Wakulima, Mifugo na Uvuvi (Nane Nane) yanayofanyika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela Nzuguni jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo aliyomwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, Mkurugenzi Wambuya alipongeza juhudi za WMA za kutoa elimu kwa wakulima, wafugaji na wajasiriamali kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi. Hata hivyo aliwataka watumishi kuongeza bidii, juhudi na maarifa katika utoaji wa huduma ili kuhakikisha huduma za uhakiki wa vipimo zinafikia wadau wote wa sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.

“Kazi yenu ni muhimu katika kulinda haki za wazalishaji na walaji. Niwahimize muendelee na kasi hii kwa kutumia teknolojia ili kila mkulima na mfanyabiashara apate uelewa na kushawishika kutumia vipimo sahihi” alisema.

Pia Mkurugenzi Wambuya alitoa wito kwa Wakala kuharakisha michakato ya utekelezaji wa huduma mpya za kivipimo zilizopangwa na Serikali ili zianze kutoa manufaa kwa wananchi mara moja.

Alisisitiza kuwa Serikali imeweka nguvu katika kuboresha sekta ya vipimo ili kuongeza tija na ushindani wa bidhaa za Kitanzania sokoni ndani na nje ya nchi.



No comments:

Post a Comment