RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli hataweza kuhudhuria mchezo wa soka kati ya Tanzania na Algeria kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Badala
 yake, Makamu wa Rais, Dk. Samia Hassan Suluhu ndiye atakuwa mgeni rasmi
 katika mchezo huo wa kwanza Raundi ya Pili kufuzu Kombe la Dunia mwaka 
2018 Urusi.
 
Hiyo
 inafuatia Rais Magufuli kufiwa na mjukuu wake, Maryfaustna Mlyambina, 
aliyefariki Novemba 11, 2015 Kimara mjini Dar es Salaam na jana 
kusafirishwa mkoani Mwanza kwa mazishi. 
Lakini
 taarifa zinasema Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais Mstaafu, Dk. Jakaya 
Mrisho Kikwete naye atakuwepo leo Uwanja wa Taifa kuongoza hamasa kwa 
wachezaji waifunge Algeria.
Mchezo wa kesho utakuwa wa nane kihistoria kuzikutanisha timu hizo, Tanzania ikishinda mara moja, kutoa sare tatu na kufungwa tatu.
 
![]()  | 
| Rais Dk John Pombe Joseph Magufuli amefiwa na mjukuu wake, hivyo hatakuwepo Uwanja wa Taifa leo | 
Mchezo wa kesho utakuwa wa nane kihistoria kuzikutanisha timu hizo, Tanzania ikishinda mara moja, kutoa sare tatu na kufungwa tatu.
Taifa
 Stars iliifunga Algeria Januari 21 mwaka 1995 Uwanja wa Taifa, Dar es 
Salaam kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizofanyika mwaka 
1996 Afrika Kusini wakati marudiano Algeria ilishinda 2-1 Julai 28, 
mwaka 1995 mjini Algiers, hiyo ilikuwa hatua ya makundi ya mtoano.
 
Kabla
 ya hapo, timu hizo zilikutana mara ya kwanza kabisa katika Michezo ya 
Afrika (All Africans Games) mjini Lagos, Nigeria Januari 8, mwaka 1973 
na  Algeria ikashinda 4-2.
 
Timu
 hizo zikaja kukutana tena katika mchezo wa michuano ya ufunguzi wa 
Uwanja wa Uhuru baada ya ukarabati, iliyopewa jina Kombe la Sumaye na 
Algeria ikashinda 1-0 Dar es Salaam Oktoba 4, mwaka 1997.
 
Timu
 hizo zikaja kukutana tena katika mechi ya kirafiki ya kimataifa Agosti 
18 mwaka 2002 na kutoa sare ya bila kufungana Uwanja wa Taifa, Dar es 
Salaam.
 
Zikakutana
 tena Septemba 3, mwaka 2010 kuwania tiketi ya Mataifa ya Afrika na 
kutoa sare ya 0-0 Algiers wakati marudiano Septemba 3 mwaka 2011, timu 
hizo zikatoa tena sare ya 1-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na huo 
ndiyo ulikuwa mchezo wa mwisho timu hizo kukutana.
 
Baada
 ya mchezo wa leo timu hizo zitarudiana mjini Algiers Jumanne na 
mshindi wa jumla atakwenda hatua ya makundi ambayo itakuwa ya mwisho ya 
mchujo katika mbio za Urusi 2018.


No comments:
Post a Comment