
November 25 umefanyika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambapo kwa Dodoma yalifanyika katika viwanja vya Nyerere square huku mgeni rasmi akiwa ni mkuu wa wilaya ya Dodoma Christina Mndeme.
Moja ya tukio lililogusa hisia za wengi ni simulizi ya mwanafunzi Joyce Samwel aliyebakwa na mwalimu wake na kisha kumsababishia ujauzito uliopelekea kukatisha masomo yake..
‘Nilipofika
 darasa la saba mwalimu Mtajama aliniita ofisini kwake akaniambia 
ananipenda nikamkatalia na kumwambia mimi nataka kuendelea na masomo 
akaniambia kama ni kusoma shule nitasomatu‘- Joyce Samwel
‘Nikamuuliza je, nikipata 
mimba itakuwaje akaniambia nisiwe na wasiwasi nikipata ujauzito 
tutalitatua, siku ya pili aliniita nyumbani kwake na nilivyoenda 
akanivuta chumbani kwake na kunivua sketi‘ –Joyce Samwel
‘Baadae
 alinilaza kwenye kitanda chake na kuniingilia kimwili na baadae 
nikapata ujauzito, nilivyomtaalifu akasema ataongea na wazazi wangu 
hivyo nisiwe na wasiwasi‘ –Joyce Samwel
Unaweza kuendelea kumsikiliza kwenye hii video hapa chini…..
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment