Hiki ndicho unapaswa kufahamu baada ya timu 32 kuelekea kombe la dunia kukamilika - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Thursday, November 16, 2017

Hiki ndicho unapaswa kufahamu baada ya timu 32 kuelekea kombe la dunia kukamilika



Peru limekuwa taifa la mwisho kukata tiketi kwenda kushiriki michuano ya kombe la dunia itakayopigwa mwakani nchini Urusi baada ya kuibuka kidedea kwa mabao 2 kwa 0 zidi ya New Zealand.

Nini kinafuata? Baada ya mataifa 32 kufudhu sasa kinachofuatia ni droo ya kupanga timu hizo 32 katika makundi kwa ajili ya fainali hizo, mchezo ambao utafanyika siku ya kesho Ijumaa mjini Moscow.

Wababe, Timu za Ubelgiji, Hispania na Uingereza ndio timu ambazo zimefudhu katika michuano hiyo bila kupoteza mchezo hata mmoja na ndio timu pekee ambazo zimeingia katika michuano hiyo kwa kishindo.

Timu ya taifa ya Brazil haikuanza vizuri kampeni za kufuzu kwani walishinda mchezo mmoja kati ya sita ya mwanzo lakini baada ya kuja kocha mpya Tite ndipo wakaanza kupata matokeo mazuri wakishinda mechi 10 na kusuluhu 2 kati ya 12.

Timu zitapangwa kutokana na viwango vya shirikisho la soka vilivyotangazwa mwezi uliopita, makundi hayo yanatangwazwa kutoka kwenye magroup 4 ambayo tayari yamepatikana baada ya michezo ya kufudhu.

Suprise, Wakati hao wakiwa na rekodi ya kufuzu kwa kishindo kuna mataifa ambayo hii itakuwa mara yao ya kwanza kushiriki michuano ya kombe la dunia, Iceland hii ni michuano yao ya yakwanza huku pia Panama wakienda kombe la dunia kwa mara ya kwanza.

Mshtuko, kuna mshtuko pia kuelekea michuano hii haswa taifa la Italia kukosa michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu 1958, ukiacha Italia kuna Mexico, Ivory Coast, Ghana na Cameroon pia ni mataifa makubwa yaliyokosa michuano hii.

TIKETI, hadi sasa FIFA wanasema kuna maombi milioni 3.5 ya tiketi za kombe la dunia huku kati ya hizo kuna 300,000 tayari zimeshafanyiwa application kwa ajili ya mechi ya fainali . 57% ya walioomba tiketi hizo wanatokeoa Urusi huku tiketi ya bei rahisi ni £345.

No comments:

Post a Comment