Kampeni ya uanzishwaji viwanda vidogo kila mkoa yazinduliwa Dodoma,,,,,,,,,,,,,,,, - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Friday, November 10, 2017

Kampeni ya uanzishwaji viwanda vidogo kila mkoa yazinduliwa Dodoma,,,,,,,,,,,,,,,,


Waziri wanchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Seleman Jafo amezindua rasmi kampeni ya uanzishaji wa viwanda vidogo na vya kati kila mkoa kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi ifikapo 2020.

Uzinduzi huo umefanyika Mjini Dodoma ambapo waziri TAMISEMI Sememani Jafo amesema lengo hilo litafanikiwa endapo watendaji wake watafanya kazi kwa weledi na kusema kuwa wizara yake itaandaa mazingira rafiki yatakayowezesha utekelezaji wa azma hiyo.

Waziri wan chi ofisi ya waziri mkuu anayesimamia sera ,bunge kazi ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama,amesema  serikali imejipanga kuwajengea wananchi ujuzi wa kuingia katika uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake naibu waziri viwanda ,biashara na uwekezaji mhandisi stella manyanya amewatoa hofu wakuu wa mikoa juu ya namna ya kutekeleza  suala hilo..

Kaulimbiu ya kampeni ya uanzishwaji wa viwanda 100 kila mkoa inasema,mkoa wetu,viwanda vyetu.

Hii ni baada ya kutolewa maagizo ya serikali kuhusu uanzishwaji wa viwanda 100 vidogo na vya kati  kila mkoa ,ambapo uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika rasmi kitaifa.

No comments:

Post a Comment