Lema atoa neno kwa RC Gambo - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Saturday, November 25, 2017

Lema atoa neno kwa RC Gambo



Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kutojaribu kufanya hila zozote za kuisababishia CCM ipate ushindi kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika hapo kesho, Novemba 26.

Lema amesema kwamba anafahamu kila hatua na vikao ambavyo Mkuu huyo wa Mkoa na kwamba ana ushahidi wa kutosha wa kila kitu kinachopangwa.

“Mrisho Gambo, unapaswa kujua kwamba huna mamlaka wala uwezo wa kushinda huu uchaguzi kwa nguvu/hila, hakuna kikao umekaa ambacho sina taarifa zake na ushahidi wa kila kitu” amesema  Lema.

Hata hivyo, Lema ameongeza kwa kumkanya kiongozi huyo asijaribu kufanya hivyo.
“Unataka kushinda uchaguzi huu kwa gharama yoyete ile? sababu polisi wako nyuma yako? usijaribu” Lema ameandika kupitia ukurasa wake wa Twitter asubuhi ya leo.

Kesho Novemba 26, mwaka huu kata 43 zinatarajiwa kufanya uchaguzi wa marudio wa kuwapata madiwani.

No comments:

Post a Comment