Miamba ya nchini Hispania Real Madrid baada ya kumkosa golikipa wa Manchester United David De Gea sasa wamerudi tena katika klabu hiyo kwa ajili ya kujaribu kufanya usajili wa mchezaji mwingine.
Mkataba wa Juan Mata na Manchester United unakaribia kuisha hivyo ni wazi United wanaweza kuvutiwa na kiasi cha pesa ambacho kitatolewa na Madrid kama ada ya kumnunua Juan Mata.
Juan Mata pia anaweza kuvutiwa na dili la kurudi nchini Hispania kwani msimu huu amekuwa hapewi dakika 90 uwanjani huku akifanikiwa kuanza katika michezo 11 kati ya 12 msimu huu.
Toka Juan Mata acheze katika mchezo ambao Manchester United walifungwa bao 2 kwa 1 na Huddersfield amekuwa akikaa nje huku mchezo pekee aliocheza baada ya mchezo huo ni mechi ya Champions League dhidi ya Benfica.

Historia kati ya Jose Mourinho na Juan Mata sio nzuri kwani mwanzo Jose alimuuza akiwa Chelsea na sasa inaonekana haitakuwa ngumu kwa kocha huyo wa United kumuuza tena kiungo huyu wa Hispania.
No comments:
Post a Comment